Machapisho
1 . KUPIGA VITA VIZURI VYA IMANI DHIDI YA JESHI OVU LA HILA ZA SHETANI
Kitabu hiki chenye kurasa zaidi ya mia moja hamsini kina mambo makuu 8 yasiyoweza kupuuzwa na mtu yeyote anayepumua hapa duniani.
1. Kimeelezea kwa kina kuhusu majeshi maovu ya hila za shetani ambayo yametumwa na kusambazwa hapa duniani kwa kazi maalumu yakuliangamiza kanisa. Kimeyafunua wazi majeshi 31 ambayo ibilisi ameyatuma hapa duniani toka kuzimu.
Haya ni maelezo kwa kifupi kuhusu baadhi ya maagizo maovu juu ya majeshiya ibilisi yakiamriwa na shetani mwenyewe Jeshi ovu la mafarakano- Shetani alitokea mbele ya jeshi hili akaliagiza nakuliambia huku akionesha msisitizo na umakini akasema-Nendeni mkafarakanishe maana mimi sitaki umoja. Mnafahamu , umoja wao ni mkuki unaonipiga ubavuni na kunifanya kulegea.
Ninawatuma nyie mkashambulie mahali popote penye umoja. Alipo maliza kusema hayo, akalipita jeshi hili kuelekea lingine.
Haya mapepo yanapoondoka kutenda kazi yanaenda taratibu yakiwa yametoa macho kwa umakini wa hali ya juu sana, kuangalia wapi kuna umoja.
Jeshi la uadui- Shetani alitokea mbele ya jeshi hili akaliagiza akasema:- Nendenimkasababishe kazi yenu kuonekana kila mahali (uadui) mtakaposababisha hiyo kazi kuonekana ndipo tutafanikiwa kusababisha mgawanyiko; kitu ambacho kitasaidia sisi kuwafanya wasiwe na ile hali ya kushirikiana ilituweze kusababisha uharibifu wetu kwa raha sana bila kubugudhiwa wala kuzuiliwa na yeyote. Baada ya hayo maagizo, shetani alisonga mbele zaidi kwenye majeshi mengine.
Jeshi lakuandaa watoto wakristo kuwa watumishi wa shetani-Alipofika shetani kwenye jeshi hili aliyageuza macho yake huku na huku akiliangalia jeshi hili kwa mkazo, kana kwamba anahisi kuna mapepo yamepungua kwenye hili jeshi ndipo akaliambia;- myaenda kufanya kazi yangua hii, bila haraka lakini kwakumaanisha .
Nawapa vifaa na nyenzo, zitakazo wawezesha kuhakikisha mtoto asilelewe na kukuzwa katika maadili sahihi ya Mungu wao.Japokuwa kazi yenu ni ya muda mrefu lakini inafaida kwangu kwa kuwa napata jeshi litakalonitumikia kwa nguvu. " Akiisha kusema hayo akaondoka. Jeshi hili lilielekezwa kwa watoto wenye umri wa kuanzia miaka 12 hadi 23.
NB: Jitahidi upate kitabu hiki, utapata mambo mengu ndani yake.
NB: Jitahidi upate kitabu hiki, utapata mambo mengu ndani yake.
2 . MAOMBI YAKUSAMBARATISHA MAJESHI YA ROHO ZA KICHAWI.
Kitabu hiki kina kurasa zaidi ya mia moja na thelathini.
Kitabu hiki kina mambo mengi mazuri yaliyo ya muhimu sana kwa kila mtu anayetaka kuishi duniani akiwa mshindi dhidi ya ya majeshi haya sumbufu ya roho za kichaw Kimeelezea wazi baadhi ya makundi matatu ya watu wanaoishi hapa duniani, kwamba kundi la kwanza ni watu ambao wanaishi kwa kubahatisha yaani wanaishi katika namna ambayo, wachawi wanapoamua kuwafanyia kitu chochote wanawezakufanya katika kundi hili wapo maskini, matajiri, wasomi n.k.
Ni katika hili kundi ndipo wachawi huchagua watu wakuwatoa makafara na kuwafanya kuwa watumwa wakichawi bila wahusika kujijua hata kidogo. Kundi la pili ni lile la watu wanaoishi duniani kwa kujitahidi. wanaishi kwa kusumbuliwa na wachawi japo hawashindwi moja kwa moja. Hawa ni watu ambao wanaelewa fika kwamba wachawi wamewazuilia baraka zao , lakini hawajui lakufanya. Mara nyingi hushambuliwa na wachawi usiku wakiwa usingizini au wakiwa macho.
Kundi la tatu ni lile ambalo linaogopwa sana na wachawi. Hili kundi ni kundi sumbufu sana kwakuwa hata wachawi wenyeqe na bosi wao shetani wanalifahamu kundi hili. Shetani analiogopa kundi hili japo haachi kulijaribu kwa maana yeye ni mjaribu. Ni kundi ambalo linaonekana kama mianga ya moto duniani.
Kitabu hiki kimeelezea kwa kina jinsi ambavyo unaweza ukawa mmoja wa watu wa kundi hili sumbufu kwa wachawi .Mapambazuko ya alifajiri moja ya tarehe 14.11.2011 saa 12:55 usiku siku ya Jumapili ndipo mtumishi huyu Mwalimu na Mtume Alam Kayengela alipoletewa ujumbe huu mahususi.
Yapo mambo mengi sana utakayojifunza ndani ya kitabu hiki.
Kitabu hiki chanya kurasa zaidi ya mia moja na kumi. kimesheheni hazina nyingi sana za masomo yasiyopungua thelathini yanayomfanya mtu kwa namna yoyote ajitambue kwa undania sana yeye ni nani ndani ya Kristo Yesu. Katika kitabu cha Yohana 1: 19-34 mafarisayo walituma watu kumuuliza Yohana ilikujua yeye ni nani. Utambulisho wake ulidhihirisha wazi jinsi yeye binafsi alivyokuwa anajitambua kwamba yeye ni nani ndani ya Kristo yesu.
Kitabu hiki kimeelezea kwa kina jinsi ambavyo unaweza ukawa mmoja wa watu wa kundi hili sumbufu kwa wachawi .Mapambazuko ya alifajiri moja ya tarehe 14.11.2011 saa 12:55 usiku siku ya Jumapili ndipo mtumishi huyu Mwalimu na Mtume Alam Kayengela alipoletewa ujumbe huu mahususi.
Yapo mambo mengi sana utakayojifunza ndani ya kitabu hiki.
3 . CHUKUA NAFASI YA KUJITAMBUA WEWE NI NANI NDANI YA KRISTO.
Kitabu hiki chanya kurasa zaidi ya mia moja na kumi. kimesheheni hazina nyingi sana za masomo yasiyopungua thelathini yanayomfanya mtu kwa namna yoyote ajitambue kwa undania sana yeye ni nani ndani ya Kristo Yesu. Katika kitabu cha Yohana 1: 19-34 mafarisayo walituma watu kumuuliza Yohana ilikujua yeye ni nani. Utambulisho wake ulidhihirisha wazi jinsi yeye binafsi alivyokuwa anajitambua kwamba yeye ni nani ndani ya Kristo yesu.
Walimuuliza - Wewe ni Eliya? Akasema hapana. Wewe ni Yesu? Akasema hapana.- na kadhalika. Baadae aliwajibu nakuwaambia" mimi nisauti ya mtu aliye nyikani, inyoosheni njia ni njia ya bwana..." Je! Kwanini hakusema mimi ni Yohana mwana wa Zakaria? Hapa alikuwa anatuonesha wazi jinsi yeye mwenyewe alivyojitambua ni nani ndani ya Kristo.
Baada yakukisoma kitabu hiki utajigundua kwamba wewe ni zaidi ya vile ulivyojifahamu. Utapata mwinuko mpya waliroho kwakusoma kitabu hiki cha kuchukua nafasi yakujitambua wewe ni nani ndani ya kristo. Utafahamu mengi kujihusu wewe kupitia masomo haya 30 yakujitambua wewe ni nani ndani ya Kristo Yesu, yaliyofunuliwa kwenye kitabu hiki cha muhimu na cha lazima kwa kila mtu.
Kitabu cha haya ni maombi yaliyothibitishwa kinakuwa sasa ni kitabu cha aina tofauti na vile mtu anavyoweza kukidhania ikiwa baada yakukisoma. Pindi utakapoanza kusogeza kurasa moja baada ya nyingine kwa kusoma kitabu hiki, haraka utagundua kwamba, ni kitabu kinachohusu maombi lakini kikiwa si cha kawaida. Ndiyo! Hilo unaweza kulitarajia.Kitabu hiki kimetoa maelekezo sahihi na kwa uwazi , jinsi unavyoweza kutembea na Mungu katika wingu la upako wa maombi mwaka huu.
Kimefafanua mambo mengi yakuhusu maombi mfano ni maombi ya aina ganai unayotakiwa kuwa nayo unapoanza mwaka , mwezi ,wiki, siku hadi saa.Kimetoa muongozo pia katika mambo yafuatayo;
Mwaka wenye miezi kumi na mbili unatakiwa uombe siku ngapi?
Baada yakukisoma kitabu hiki utajigundua kwamba wewe ni zaidi ya vile ulivyojifahamu. Utapata mwinuko mpya waliroho kwakusoma kitabu hiki cha kuchukua nafasi yakujitambua wewe ni nani ndani ya kristo. Utafahamu mengi kujihusu wewe kupitia masomo haya 30 yakujitambua wewe ni nani ndani ya Kristo Yesu, yaliyofunuliwa kwenye kitabu hiki cha muhimu na cha lazima kwa kila mtu.
4 . HAYA NI MAOMBI YALIYOTHIBITISHWA
(MWILI WAKO NI MNYORORO MKUU UNAOKUFUNGA USIWEZEKUTEMBEA NA MUNGU KATIKA WINGU LA UPAKO WA MAOMBI MWAKA HUU)
Kitabu cha haya ni maombi yaliyothibitishwa kinakuwa sasa ni kitabu cha aina tofauti na vile mtu anavyoweza kukidhania ikiwa baada yakukisoma. Pindi utakapoanza kusogeza kurasa moja baada ya nyingine kwa kusoma kitabu hiki, haraka utagundua kwamba, ni kitabu kinachohusu maombi lakini kikiwa si cha kawaida. Ndiyo! Hilo unaweza kulitarajia.Kitabu hiki kimetoa maelekezo sahihi na kwa uwazi , jinsi unavyoweza kutembea na Mungu katika wingu la upako wa maombi mwaka huu.
Kimefafanua mambo mengi yakuhusu maombi mfano ni maombi ya aina ganai unayotakiwa kuwa nayo unapoanza mwaka , mwezi ,wiki, siku hadi saa.Kimetoa muongozo pia katika mambo yafuatayo;
Mwaka wenye miezi kumi na mbili unatakiwa uombe siku ngapi?
- Mwezi wenye siku 30 au 31 unatakiwa uombe siku ngapi?
- Wiki yenye siku saba unatakiwa uombe siku ngapi?
- Siku yenye saa 24 unatakiwa uombe muda gani?
- Masaa yenye dakika 60 unatakiwa utumie muda gani katika kuomba.
Ndani ya kitabu hiki pia yameainishwa mambo yanayoweza kuwa kikwazo na kizuizi cha majibu ya maombi yako.
Kila mtu anahitaji hiki kitabu.
(sauti ya Roho mtakatifu ya maonyo kwa wachungaji na awatumishi wote wa kizazi hiki ulimwenguni).
Tarehe 18.09.2011 siku ya Jumamosi saa 2:00 asubuhi ndipo Mungu alipomletea ujumbe huu mtumishi wa Mungu na kupewa agizo la kuandika na kuweka kwenye jarida chache za kitabu hiki.
Ujumbe huu alipoupata mtumishi wa Mungu ulimfanya Kuugua Rohoni karibu wiki mbili , hasa anapokumbuka msisitizo wa maonyo ya roho Mtakatifu kwa wachungaji na watumishi wote wa kizazi hiki ulimwenguni. mara nyingi aliandika kitabu hiki akiwa analia machozi. Kitabu hiki kina maonyo tisa tu ambayo mtumishi wa Mungu aliyaandika moja baada ya jingine kwakusikiliza kwa makini asije akaandika tofauti na yale ambayo Roho wa Mungu angetaka yawafikie kwa ukamilifu watumishi wa Mungu
wote wa kizazi hiki ulimwenguni. KILA MCHUNGAJI AKIPATE KITABU HIKI.
Kila aliyekipata kitabu hiki anaweza akakiri wazi kwamba ,siyo mawazo ya mwandishi aliyepangilia kwa utaalamu usio wakawaida maneno ya kitabu hiki.
5 . KUITAMBUA SAUTI TYA MUNGU.
(sauti ya Roho mtakatifu ya maonyo kwa wachungaji na awatumishi wote wa kizazi hiki ulimwenguni).
Tarehe 18.09.2011 siku ya Jumamosi saa 2:00 asubuhi ndipo Mungu alipomletea ujumbe huu mtumishi wa Mungu na kupewa agizo la kuandika na kuweka kwenye jarida chache za kitabu hiki.
Ujumbe huu alipoupata mtumishi wa Mungu ulimfanya Kuugua Rohoni karibu wiki mbili , hasa anapokumbuka msisitizo wa maonyo ya roho Mtakatifu kwa wachungaji na watumishi wote wa kizazi hiki ulimwenguni. mara nyingi aliandika kitabu hiki akiwa analia machozi. Kitabu hiki kina maonyo tisa tu ambayo mtumishi wa Mungu aliyaandika moja baada ya jingine kwakusikiliza kwa makini asije akaandika tofauti na yale ambayo Roho wa Mungu angetaka yawafikie kwa ukamilifu watumishi wa Mungu
wote wa kizazi hiki ulimwenguni. KILA MCHUNGAJI AKIPATE KITABU HIKI.
Kila aliyekipata kitabu hiki anaweza akakiri wazi kwamba ,siyo mawazo ya mwandishi aliyepangilia kwa utaalamu usio wakawaida maneno ya kitabu hiki.
- Unapoanza kusoma kitabuhiki mwanzo mpaka mwisho, unakuwa umeshaielewa sauti ya Mungu inayokuwa inazungumza na wewe kupitia kitabu hiki.
- Hii ni dalili ya Mungu kuwapenda watumishi wake wakizazi hiki ulimwenguni, kwamba anaweza akawaonya .- Huu ni upendo .
NB: Kila mtumishi akipate kitabu hiki.
6 . ZITAMBUE BAADHI YA ROHO 76 ZINAZOTESA KIZAZI HIKI.
Kitabu hiki ni kitabu maalumu kilichobainisha baadhi ya roho 76 zinazotesa kizazi hiki.
Baadhi ya hizo roho 76 zinazotesa kizazi hiki , ziliwahi kutesa pia vizazi vingi vya mwanadamu tangu alipowekwa duniani katika karne zilizopita.
Roho zote 76 zilizofunuliwa katika kitabu hiki, zimewekwa wazi kwa Neno kila roho ikifunuliwa na andiko jinsi ilivyotenda kazi kwa kumtumia mtu wa vizazi vile na jinsi unavyoweza ukaibainisha kwa uwazi inapotenda kazi katika kizazi chetu hiki. Mfano;- Roho ya shimei:
katika kitabu hiki hii ni roho ya 69 kati ya roho 76 zilizobainishwa katika kitabu hiki.
Unaposoma katika 25 Samweli 16: 5-14 unaona wazi mtu aliyeitwa kwa jina la
shimei jinsi alivyohusika kutukana watumishi wa Mungu, na kwakuwarushia mawe, na kujaribu kufanya ubaya wa kila namna. Roho hiyo ya shimei haikuishia hapo , katika kipindi cha Daudi bali inatenda kazi hata sasa kwa kuwatumia kina shimei wanyakati hizi za kizazi hiki. Roho hii bado inamtumia shimei kutukana na kulaani watumishi wa Mungu wakweli wakizazi hiki. Inarusha mawe ya maneno mabaya kila siku kwa watumishi wakweli wa Mungu wakizazi hiki.
Ni katika umuhimu usioweza kupuuza kwamba kitabu hiki unatakiwa kuwa nacho.
7 . BAADHI YA NJIA 30 AMBAZO MUNGU ANAZITUMIA KUSEMA NA WATU.
- Usiku wa tarehe 16..07.2010 saa 2:05 mwandishi akiwa safarini ndani ya basi alipewa ujumbe wa kitabu hiki.
- Ni kitabu kizuri sana kilicho na siri za Mungu za kumfanya mtu kwa urahisi aweze kutambua sauti ya Mungu kwa namna fulani.
- Mara utakapokuwa umesoma kitabu hiki na kukimaliza kwa usahihi utaanza mwenyewe kupata uhakika wa dhati kwamba unaweza kusikia Munu akiongea na wewe aidha kwa njia ambayo hapo kabla hukuijua.
- Muhtasari mfupi wa kitabu hiki - hebu ukupe hali yakujua kwamba kwa namna yoyote ile kitabu hiki, kimeshehenii hazina nzuri zilizo za Mungu kwako binafsi.
- Asilimia kubwa sana ya idadi ya wakristo humu ulimwenguni waliowahi kuishi na wale waliopo mwelekeo wa ufahamu wao kuhusu njia ambazo Mungu huzitumia kusema na watu ni kama zifuatazo;
- Sauti ya wazi
- Kwa njia ya ndoto
- Kwa njia ya maono
- Kwa njia ya dhamiri au amani ya Kristo
- Kwa njia ya manabii au malaika
- Hizo ni baadhi ya njia ambazo watu wanhisi kuwa Mungu anawezakuzitumia kusema nao.
- Njia zingine 25 bado zimesitirika lakini kitabu hiki kimeweka wazi njia hizo kwa usahihi zaidi.
8 . CHUKUA TAHADHARI JUU YA MNYAMA KATILI ACHINJAE NA KUANGAMIZA (KIBURI).
- .Kitabu hiki kimetoa tahadhari kubwa juu ya kile kilichotafsiriwa kama mnyama katili- ambaye mnyama huyo katili ndiye kibri mwenyewe.
- Kiburi ni roho ya mnyama wa ajabu sana. Ni mnyama katili. Ni aheri utekwe na kingine chochote maana unaweza siku moja unaweza ukafunguliwa, kuliko kutekwa na mnyama huyu kiburi ambaye anakufanya Mungu kuwa kinyume chako.
- Mnyama huyu kiburi anakufanya Mungu akupinge kwa kila namna- 1 Petro 5:5.
- Ujumbe mzito ulioko ndani ya kitabu hiki,mtumishi mwalimu na mtume, Alam J. Kayengela ambaye ndiye mwandishi wa kitabu hiki, kwa neema ya Mungu alifunuliwa na Mungu tarehe 11-09-2007 akiwa Kibaha Mkoa wa Pwani kupta ujumbe huu, ujumbe wa kitabu hiki umechapwa sehemu ya kwanza hadi ya tatu.
- Kiburi ni mnyama katili mwenye mikono tisa. Ana macho makali yakuona mbali. Anaukubwa ya mfano wa Tembo. Wepesi wake wakukamata mawindo ni kama chui.
- Kitabu hiki kimeainisha wazi maeneo makuu matano ambayo mnyama huyu kiburi anapenda kutembelea ili kumkamata mtu ( mawindo).
- Pia kitau hiki kimefafanua kwa uwazi mikono tisa ambayo mnyama huyu kiburi anayotumia kuwakamatia watu (mawindo) ilikuwapokonya.
- Mungu anpokuinua juu sana hata umbali wa maili milioni kisha kwa upande wako ukajiinua mwenywe hata umbali wa futi moja tu, hiyo futi moja itaathiri umbali wote wakilele ulichokuwa umekwenda kisha maili zili zitakuwa za kwenda chini na kushushwa- haya yakiwa ni matokeo yakukamatwa na mikono yote tisa ya mnyama Kiburi.
- Kitabu hiki kwa undani zaidi kimefundisha unyenyekevu wa kweli NB:
Tahadhari usikose nakala ya kitabu hiki.
Comments
Post a Comment