Leoleoplus,com

MFULULIZO WA MAFUNDISHO YA APOSTLE ALAM J. KAYENGELA KWENYE KONGAMANO LA SIKU NANE ARUSHA TANZANIA (TAREHE 5-12 MWAKA 2013)


        
       
SIKU YA 4:
·         MIUNGU YA YEZEBELI NA KIZAZI HIKI.
-          Yezebeli alizaliwa katika familia ya waabudu miungu, wasiomuabudu BWANA MUNGU ALIYEHAI. Baba yake aliitwa Ethbaal ambaye alikuwa Mfalme wa Sidoni. Yezebeli alikuwa na muunga niko wa kishetani tokea akiwa kwa baba yake. Ethbaal babayake Yezebeli kama jina lake lilivyo, alikuwa moja kwa moja amejiunganisha na milango ya kuzimu – hata jina lake akaliunganisha na miungu aliyoiabudu na kuitumikia. Alikuwa mchawi na mshirikina wa viwango. Baada ya miaka 38 ya utawala wa Mfalme Asa, katka Israel – Ahabu alichukua kiti cha ufalme. Ahabu alitafuta mke na kumuoa Yezebeli binti wa Ethbaal aliyekuwamchawi namwenye ibada bandia za kishetani – Ifalme 16:29 – 31.

-          Yezebeli katika kiwango cha uchawi alichokuwa amekifikia, alipewa heshima na shetani kuwa kama malkia wa kuzimu katika mamlaka ya giza. Alikuwa mzinzi na mwenye uchawi mwingi sana – 2 Falme 9:22. Yezebeli kwa hila kubwa ya kichawi, alijiita nabii wa Mungu na kwa utambulisho huo akafanikiwa kuwaangusha wana wa Israeli na watumishi wengi wengi wa Mungu kwenye uzinzi – Ufunuo 2:20.

Yezebeli ndiye aliyemuongoza mume wake katika kila jmabo, uchawi aliokuwa nao ulimeza maamuzi ya Ahabu mume wake. Yezebeli aliendesha oparesheni za kuwaoa na kuwachinja manabii wa Bwana – 1Falme 18:4 lengo lake ilikuwa kulisambaza lile giza la uovu katika nchi yote ya Israeli Mts 19 Yezebeli alikuwa na mtandao mkubwa wa miungu aliyoitumikia na kuimiliki – ukisoma katika 1Falme 18:19 miungu ya baal miungu ya Ashera na muingu ya baal – peori – Hes. 25: 1 – 3 n.k. Mtandao huo ulimfanya kuwa mwanamke hatari katika ulimwengu waroho na mwili. Jamii ili muogopa na kumuhofu, alichokiamua ndicho alitenda,na ndicho kilicho tendeka.

·         Utajuaje una roho za miungu ya Yezebeli?
-          Tafakari vizuri 2 Wafalme 9:30 na Yer 4;30 “………..Yezebeli akapata habari, akatia wanja machoni pake, akapamba kichwa chake……….. ujapo jivika mavazi mekundu, ujapo jipamba mapambo ya dhahabu, ujapojitia wanja machoni, unajifanya kuwa mzuri bure tu ……..”
1.       Kutaka kumuongoza mume wako
2.       Kuvaa mavazi ambayo aina ya mshono au fasheni yake imewekwa wakfu kwa miungu
3.       Kupaka wanja – nyusi, mdomo n.k.
4.       Kuvaa nywele za bandia
Kila anayeshawishiwa na vitu hivyo bila kujali yeye ni nani – bado hajaepuka miungu ya Yezebeli. Tabia za miungu ya Yezebeli sasa zimejieneza na kuonekana kusonga mbele hata kwenye nyumba ya Mungu.










Wanaofuata nyayo za Yezebeli kwa makusudi – ni wengi, lakini pia wanaofuata tabia za kiyezebeli pasipo wao kujua wala kukusudia – ni wengi.

-          Utajuaje kwamba unafuata tabia za Yezebeli kwa makusudi? -Ukionywa ili uache hiyo tabia unakaidi na kukasirika, kama vile vile Yezebeli alivyokuwa anafanya. Alimkasirikia mtu yeyote aliyejaribu kumkosoa.

-          Utajuaje kwamba unafuata roho za miungu ya Yezebeli pasipo kujua wala kukusudia? Ukionywa tu juu ya tabia hizo za kiyezebeli mara moja unaacha. Ni rahisi tu, kama hivyo.

·         Kifo cha mtu anayeandama miungu ya roho ya Yezebeli.
Angalia 2 Wafalme 9: 30 – 37
1.       Kwanza unakuwa mwanamke uliyelaaniwa kwa sababu ya tabia hizo za roho za miungu ya Yezebeli – Mst 34
2.       Unakufa kifo cha aibu – Mst 33 – 36 na unaweza ukafa kifo cha kumwagika damu si kwa sababu una dhambi zingine “Hapana” bali ni kwa vile unavyoandama roho za miungu ya Yezebeli kwa tabia zake unazo zipendelea.
3.       Kifo chako hakitawasikitisha watu wengi isipokuwa husema – bora ameondoka.

MAOMBI:
1.       Mungu Baba mwenye pendo, nakupenda, nakupenda, nakupenda sana. Naam Bwana Yesu wewe ni zaidi, unanipenda kupita upeo. Nisamehe kwani kuna wakati nimekuwa nikiandama roho za miungu ya Yezebeli.
2.       Kila roho ya Yezebeli inayonijia usingizini kama nyokaleo, Roho mtakatifu anaipiga radi toka mbinguni – kwa jina laYesu Kristo.
3.       Roho za miungu ya Yezebeli na kupiga stop. Koma kunifuatilia. Simama hapo hapo ulipo na ugande kama friji – Kwa jina la Yesu Kristo.
4.       Mawe yamoto kutoka mbinguni shusha kipigo kwa miungu ya kiyezebeli inayo niondo lea heshima ya kiMungu maishani mwangu-Katika Jina la Yesu Kristo
5.       Sura yangu, mwili, wangu, nguo zangu, kataa kushirikiana na roho za miungu ya Yezebeli – katika Jina la Yesu Kristo.

ZINGATIA MAELEZO HAYA:
1.      Kama bado unasikia moyoni mwako kueendelea kushirikiana na bidhaa za Yezebeli ambazo zimebeba miungu ya Yezebeli – mfano – kupaka wanja, kupaka rangi kwenye kucha na kupendelea nywele za bandia, ``` kiasi kwamba unaona ugumu kuviacha vitu hivyo – chukua siku 3 mfululizo ufanye maombi ya kuchoma kwa moto bidhaa za miungu ya Yezebeli  zilizoko ndani yako.
2.      Wakati mwingine tunalazimika kuviacha vile tunavyo vipenda ilimradi tu, havimletei Mungu heshima. Chochote ambacho Mungu hajaturuhusu kwenye neno lake siyo chetu, bali ni vya ulimwengu.
3.      Bila kujali utaonekanaje katika jamii inayokuzunguka, unalazimika kumsikiliza Roho mtakatifu anayekusihi kwa sauti ya upendo ili uachane kabisa na namna yoyote ya kiyezebeli, ambayo kwa muda mrefu – imekupunguzia uwepo wa Mungu.

v  ONYO!!!
Umekatazwa kutoa copy ujumbe ulioko kwenye karatasi hii ili kumpa mwingine,isipokuwa umeruhusiwa kumchukulia rafiki yako karatasi yake mwenyewe. Itakuwa dhambi ya makusudi ya kutokutii usipo zingatia onyo hili.

AMINA!!!!.

Comments

Popular posts from this blog

NENO LAUFUNUO LA LEO tazama Ayubu 8:7"Tena ujapokuwa huo mwanzo wako ulikuwa mdogo,lakini mwisho wako ungeongezeka sana"NENO LA UFUNUO LASIKU YAKO LEO. MUNGU ANAKUTAKA USIWE NAMAWAZO YA KUDHARAU MWANZO WAKOMDOGO. KWAMAANA TABIA YA MUNGU NIKWAMBA,YEYE HUWA HAUDHARAUMWANZO MDOGO. HATAKAMA NIMWANZO MDOGO YEYE HATAUDHARAU. "Mungu alianza na mwanadamu mmoja,leo hii wako mabilioni. Yesu alianza na wanafunzi kumi nawawili,leohii anawafuasi wengi hata hawana idadi maanawengine walishatangulia mbinguni. Historia yamakanisa mengi Africa na ulimwengu kwaujumla,yalianza namwazo mdogo sana lakini yamekuwa makubwa nayakushangaza."KILA MWANADAMU CHINI YAJUA ANAPITIA UZOEFU HUU WA KIPINDI CHAMWANZOMDOGO.LEO INABIDI UJIULIZE UKO KWENYEMWANZOMDOGO WAJAMBO GANI? JE UKO KWENYE MWANZOMDOGO WA KUANZISHA KAZI YAMUNGU? JE UKO KWENYEMWANZOMDOGO WANDOA? UKO KWENYEMWANZO WABIASHARA? UKO KWENYE MWANZO WA OFISI MPYA? UKO KWENYE MWANZO WAUCHUMBA? UKO KWENYE MWANZO WA AJIRA? UKO KWENYE MWANZO GANI? TAZAMA zekaria 4:10"maana ninani aliyeidharau siku yamambo madogo?.....OK. UNAONYWA! USIDHARAU MWANZO MDOGO ULIO NAO LEO. USIVUNJWE MOYO NAMWANZO MDOGO. USIKATISHWETAMAA NAMWANZO MDOGO.USIJIWAZIE VIBAYA KWASABABU YA MWANZO WAKO MDOGO. LEO,PIGA MOYO WAKO KONDE UCHANGAMKE MWISHO WAKO NIMZURI. MWISHO WAKO NIMKUBWA. POKEA NENO HILI LAUFUNUO ALILO KUTUMIA MUNGU SIKU YALEO.JITAHIDI UJE KANISANI UPATE MAELEKEZO ZAIDI. HUDUMA YA NENO LAUFUNUO CHINI YA MWANGALIZI MKUU MWL NA MTUME ARAM J.KAYENGELA IMEFANYIKA BARAKA SANA YAKIROHO NAKIMWILI KWAWOTE WALIO FANIKIWA KUJIUNGA RASMI. NIHUDUMA YAKIROHO YENYE UHUISHO MPYA KATIKA SIKU HIZI ZA HATALI AMBAZO KANISA LIMESAHAU UPENDO WAKWANZA.KANISA LIMEPOA.WATU WAKO MOTO KISIASA ILA KIROHO WAMEPOA KABISA.NINYAKATI ZA YEYE ALIYE NASIKIO AYASIKIE HAYA AMBAYO ROHO ANAYAMBIA MAKANISA.HERI MWENYE SIKIO LAKUSIKIA SASA. NIMUDA WAKO WAKUJA KWENYE NENO LAUFUNUO IKIWA ULIMUULIZA MUNGU AKUONYESHE NIWAPI UENDE. SIMAMA KWAMIGUU YAKO NAUCHUKUE HATUA. 0763359745/0712583194

SEHEMU YA PILI