Leoleoplus,com

Mtumishi

Mwalimu na Mtume Alam  J. Kayengela  ni Mkurugenzi mkuu mwanzilishi wa huduma hii.

Baada ya Mungu Kumpa  maelekezo  alimtuma toka  Mkoani Kigoma kuja kuanzisha huduma hii mnamo mwezi wa tatu mwaka 2010 Dar Es salaam katika manispaa ya Temeke eneo la Yombo Vituka.

Neno La Ufunuo:


Neno hili linatoka katika kitabu cha 1 Samweli 3:1 (b) "Na neno la Bwana lilikuwa adimu siku zile ; hapakuwa  na mafunuo dhahiri". Kama hivi tungesema mahubiri na mafundisho  yalikuwepo lakini  yakiwa hayana ufunuo.

Makuhani walitoa hotuba zao  kwa usahihi na mpangilio wa dhati, wakinukuu torati ya Musa kwa  ulinganifu  na sahihi lakini hapakuwapo na  mafunuo dhahiri.

Kwahiyo  Neno  pasipo ufunuo dhahiri ni andiko lisilo na pumzi ya Mungu 2 Timotheo 3:16 " Kila andiko lenye pumzi  ya Mungu lafaa kwa mafundisho na kwa

kuonya  watu makosa yao, na kwa kuongoza...". Hii inamaana ya wazi kwamba  kila andiko  lisilo na pumzi ya Mungu halifai kwa matumizi yoyote  ya kiroho. Hiyo ni kwa sababu andiko huua bali roho analihuisha. 


1Korintho 14:30" lakini mwingine aliyeketi akifunuliwa neno....siku zote, Neno la ufunuo mtu hupewa (hufunuliwa) na Mungu mwenyewe. Ndivyo Yesu alivyomwambia mtume Petro". Heri wewe Simoni Bar-Yona, kwakuwa mwili na damu  havikukufunulia hili ; bali Baba yangu aliye mbinguni, Mathayo 16:17". Yesu Kristo kwa kumwambia hivyo Petro alimaanisha pia kwamba, "Mwili na damu au mawazo  ya kibinadamu yanaweza kufunua mahubiri japo yanakuwa hayana nguvu ya kumpa  mtu uhai". Ila kumdumaza mtu kiroho na kimwili.



Huduma ya Neno la ufunuo ya Uongozi wa Roho Mtakatifu kupitia Mwalimu na Mtume Alam J. Kayengela ianshughulika  na haya yafuatayo:-


1. Kumfanya mtu alijue neno la Mungu kwa usahihi wa kina.

2. Kumfanya mtu abadilishwe na neno kiroho na kimwili.

3. Kumfanya mtu aliishi neno kila siku.

4. Kumfanya mtu awe na uwezo binafsi wakupata mahitaji yake kutoka kwa Mungu

kupitia neno la ufunuo.

5. Kumfanya mtu awe na ufahamu pevu kuhusu Mungu wa kweli anemwabudu na

kumtumikia.

6. Kumfanya mtu kuwa na uwezo binafsi wakuishi bila kuathiriwa na mwovu

wakipepo chini ya jua.

7. Kumfanya mtu awe tayari mda wowote kusikia parapanda ya unyakuo.

8. Kumfanya mtu kutembea katika uokovu wa kweli.

9. Kuandaa watumishi na kuwatuma sehemu mbalimbali kwa kazi ya Mungu.

10. Huduma za Maombezi kufungua watu kutoka vifungo vya milango ya kuzimu,

kuponya magonjwa , kufungulia watu milango yakupata kazi n.k.


Mambo hayo kumi, yamekuwa halisi kwa baadhi ya watu wachache waliokubali kujiunga na huduma ya Neno La Ufunuo.

Popular posts from this blog

NENO LAUFUNUO LA LEO tazama Ayubu 8:7"Tena ujapokuwa huo mwanzo wako ulikuwa mdogo,lakini mwisho wako ungeongezeka sana"NENO LA UFUNUO LASIKU YAKO LEO. MUNGU ANAKUTAKA USIWE NAMAWAZO YA KUDHARAU MWANZO WAKOMDOGO. KWAMAANA TABIA YA MUNGU NIKWAMBA,YEYE HUWA HAUDHARAUMWANZO MDOGO. HATAKAMA NIMWANZO MDOGO YEYE HATAUDHARAU. "Mungu alianza na mwanadamu mmoja,leo hii wako mabilioni. Yesu alianza na wanafunzi kumi nawawili,leohii anawafuasi wengi hata hawana idadi maanawengine walishatangulia mbinguni. Historia yamakanisa mengi Africa na ulimwengu kwaujumla,yalianza namwazo mdogo sana lakini yamekuwa makubwa nayakushangaza."KILA MWANADAMU CHINI YAJUA ANAPITIA UZOEFU HUU WA KIPINDI CHAMWANZOMDOGO.LEO INABIDI UJIULIZE UKO KWENYEMWANZOMDOGO WAJAMBO GANI? JE UKO KWENYE MWANZOMDOGO WA KUANZISHA KAZI YAMUNGU? JE UKO KWENYEMWANZOMDOGO WANDOA? UKO KWENYEMWANZO WABIASHARA? UKO KWENYE MWANZO WA OFISI MPYA? UKO KWENYE MWANZO WAUCHUMBA? UKO KWENYE MWANZO WA AJIRA? UKO KWENYE MWANZO GANI? TAZAMA zekaria 4:10"maana ninani aliyeidharau siku yamambo madogo?.....OK. UNAONYWA! USIDHARAU MWANZO MDOGO ULIO NAO LEO. USIVUNJWE MOYO NAMWANZO MDOGO. USIKATISHWETAMAA NAMWANZO MDOGO.USIJIWAZIE VIBAYA KWASABABU YA MWANZO WAKO MDOGO. LEO,PIGA MOYO WAKO KONDE UCHANGAMKE MWISHO WAKO NIMZURI. MWISHO WAKO NIMKUBWA. POKEA NENO HILI LAUFUNUO ALILO KUTUMIA MUNGU SIKU YALEO.JITAHIDI UJE KANISANI UPATE MAELEKEZO ZAIDI. HUDUMA YA NENO LAUFUNUO CHINI YA MWANGALIZI MKUU MWL NA MTUME ARAM J.KAYENGELA IMEFANYIKA BARAKA SANA YAKIROHO NAKIMWILI KWAWOTE WALIO FANIKIWA KUJIUNGA RASMI. NIHUDUMA YAKIROHO YENYE UHUISHO MPYA KATIKA SIKU HIZI ZA HATALI AMBAZO KANISA LIMESAHAU UPENDO WAKWANZA.KANISA LIMEPOA.WATU WAKO MOTO KISIASA ILA KIROHO WAMEPOA KABISA.NINYAKATI ZA YEYE ALIYE NASIKIO AYASIKIE HAYA AMBAYO ROHO ANAYAMBIA MAKANISA.HERI MWENYE SIKIO LAKUSIKIA SASA. NIMUDA WAKO WAKUJA KWENYE NENO LAUFUNUO IKIWA ULIMUULIZA MUNGU AKUONYESHE NIWAPI UENDE. SIMAMA KWAMIGUU YAKO NAUCHUKUE HATUA. 0763359745/0712583194

MFULULIZO WA MAFUNDISHO YA APOSTLE ALAM J. KAYENGELA KWENYE KONGAMANO LA SIKU NANE ARUSHA TANZANIA (TAREHE 5-12 MWAKA 2013)

SEHEMU YA PILI