Leoleoplus,com

NENO LA UFUNUO LA WIKI HII KWA KANISA ULIMWENGUNI-Sehemu ya 3 MATOKEO YA UGONJWA WA USAHAULIFU


Msahaulifu kamwe hakuwahi kujua matokeo ya ugonjwa ule alio ambiwa na Dkt. wake [ugonjwa wa usahaulifu]

KUSOMA SHULE NZURI BILA MAFANIKIO

Msahaulifu alikuja kugundua ugonjwa wake wa usahaulifu ulivyo mbaya baada ya kutumia miaka mikgi sana shuleni bila mafanikio.

KUFERI KILA MTIHANI DARASANI

Sikumoja msahaulifu alimwita mwalimu wake pembeni,huku akiwa amenyongonyea sana na kumuuliza-Mwalimu,mimi mbona kila mtihani nimekuwa nikiferi? au labda wachawi wananisumbua?kwanini naferi kila mtihani?
Mwalimu wakati anamjibu,alimkazia macho akamnyoshea fimbo nakumwambia-Unakumbuka nimekuwa nikikuuliza uniambie ulicho jifunza unaniambia nimesahau? sasa kama unasahau ninacho kufundisha,unategemea kushinda mtihani?-kwasababu pia msahaulifu hakuwa na muda wa kutembelea daftali zake ili kujisomea yale aliyo jifunza.
Mwalimu alisikitika sana akamwambia-SASA ONA,hata mitihani midogo inakushinda
                               <itaendelea>

MAANA YA UFUNUO HUU

1.MIAKA MINGI SHULENI BILA MAFANIKIO

Niyule anaye weza kukaa kanisani miaka mingi bila kuona mafanikio kwasababu ya kuendelea kuendekeza ugonjwa huu wa usahaulifu. Ndiyo maana Mungu anaonya katika Yoshua 1;8-yatafakari maneno yake mchana na usiku
Na katika Mith 3;1-usisahau sheria yangu
pia katika 1timotheo 4;13,15 -ufanye bidii katika kusoma....."
-Mungu anacho sisitiza hapa,nikwamba hataki kabisa uwe na ugonjwa huu wa kusahau.Hataki usahau yale unayo jifunza kwasababu nihatali sana.
Kumbuka"msahaulifu alikaa kwenye shule ya viwango miaka mingi bila kuona mafanikio-kwasababu hakuwa na tabia ya kujisomea yale aliyo yaandika kwenye daftali yake,hivyo AKAWA ANASAHAU.

2.MSAHAULIFU KUFERI KILA MTIHANI DARASANI

Hii inamaanisha kwamba,unapokuwa unasahau yale ambayo Mungu anakufundisha humanisha kuwa,utashindwa pale jaribu litakapo kujia. maana majaribu ndo mitihani yakiroho. Jaribu lita kutetelesha na kuku changanya ikiwa utakuwa mwepesi wa kusahau kile ufundishwacho na Mungu.Majaribu yatakuchanganya sana kama utakuwa muathirika wa ugonjwa huu mbaya wa usahaulifu.

Unafahamu kuwa Mungu ndiye akufundishaye? japo kuwa hapo ulipo humuoni,lakini yuko kazini kuku fundisha.
-Mithali 4;2 "nawapa mafundisho mazuri ili msiiache sheria yangu
- Zab 32;8 "Nitakufundisha nakuku onyesha njia utakayo iendea"
-Isaya 48;17"Mimi ni Bwana Mungu wako nikufundishaye ili upate faida...."
-Kwanini watu wengi wanaferi mitihani ya majaribu? nikwasababu wamepatikana na ugonjwa mbaya wa kusahau kile walicho fundishwa na Mungu. Nawengine huwa hawajui kama kweli ni Mungu anaye wafundisha.

MSAHAULIFU ALIANGUSHWA NA MITIHANI MIDOGO SANA DARASANI

Mitihani hii huwa nimajaribu ambayo Mungu huyaruhusu yakufikie

Kumbu kumbu 8;3"....akakuacha uone njaa.."
-Ona. Huwa kunawakati anaamua kuku acha upitie jambo furani la kimaumivu.Hapo ndipo anataka ukumbuke kile alicho kufundisha. Hawezi kuku letea mtihani ambao hajakufundisha somo lake.
-2nyakati 32;31"...Mungu akamuacha ili amjaribu...."
Wengine hufikiri kwamba Mungu hawezi kuwajaribu. Basi atakuwa siyo mwalimu. Anapo kufundisha lazima siku moja utafanyia mtihani hayo mafunzo. Msahaulifu hakuwa anajali hilo.
 -Mitihani midogo iliyo mshinda msahaulifu-ndo yale majaribu madogo tu,ambayo huwaangusha watakatifu wengi lakini tatizo kubwa ni ule ugonjwa wa usahaulifu.

OMBA OMBI HILI

Ee Mungu uliye hai,nimetambua kwamba wewe ndio unaye nifundisha ili nipate faida,nakataa ugonja huu wa usahaulifu,kwa Jina la Yesu Kristo wa Nazaleth.

                                maombezi




 AMINA

KWAMSAADA ZAIDI WASIRIANA NASI KWA;

mlkayengela@gmail.com

alamkayengela@yahoo.com

0763359745 na 0712583194 
 

Comments

Popular posts from this blog

NENO LAUFUNUO LA LEO tazama Ayubu 8:7"Tena ujapokuwa huo mwanzo wako ulikuwa mdogo,lakini mwisho wako ungeongezeka sana"NENO LA UFUNUO LASIKU YAKO LEO. MUNGU ANAKUTAKA USIWE NAMAWAZO YA KUDHARAU MWANZO WAKOMDOGO. KWAMAANA TABIA YA MUNGU NIKWAMBA,YEYE HUWA HAUDHARAUMWANZO MDOGO. HATAKAMA NIMWANZO MDOGO YEYE HATAUDHARAU. "Mungu alianza na mwanadamu mmoja,leo hii wako mabilioni. Yesu alianza na wanafunzi kumi nawawili,leohii anawafuasi wengi hata hawana idadi maanawengine walishatangulia mbinguni. Historia yamakanisa mengi Africa na ulimwengu kwaujumla,yalianza namwazo mdogo sana lakini yamekuwa makubwa nayakushangaza."KILA MWANADAMU CHINI YAJUA ANAPITIA UZOEFU HUU WA KIPINDI CHAMWANZOMDOGO.LEO INABIDI UJIULIZE UKO KWENYEMWANZOMDOGO WAJAMBO GANI? JE UKO KWENYE MWANZOMDOGO WA KUANZISHA KAZI YAMUNGU? JE UKO KWENYEMWANZOMDOGO WANDOA? UKO KWENYEMWANZO WABIASHARA? UKO KWENYE MWANZO WA OFISI MPYA? UKO KWENYE MWANZO WAUCHUMBA? UKO KWENYE MWANZO WA AJIRA? UKO KWENYE MWANZO GANI? TAZAMA zekaria 4:10"maana ninani aliyeidharau siku yamambo madogo?.....OK. UNAONYWA! USIDHARAU MWANZO MDOGO ULIO NAO LEO. USIVUNJWE MOYO NAMWANZO MDOGO. USIKATISHWETAMAA NAMWANZO MDOGO.USIJIWAZIE VIBAYA KWASABABU YA MWANZO WAKO MDOGO. LEO,PIGA MOYO WAKO KONDE UCHANGAMKE MWISHO WAKO NIMZURI. MWISHO WAKO NIMKUBWA. POKEA NENO HILI LAUFUNUO ALILO KUTUMIA MUNGU SIKU YALEO.JITAHIDI UJE KANISANI UPATE MAELEKEZO ZAIDI. HUDUMA YA NENO LAUFUNUO CHINI YA MWANGALIZI MKUU MWL NA MTUME ARAM J.KAYENGELA IMEFANYIKA BARAKA SANA YAKIROHO NAKIMWILI KWAWOTE WALIO FANIKIWA KUJIUNGA RASMI. NIHUDUMA YAKIROHO YENYE UHUISHO MPYA KATIKA SIKU HIZI ZA HATALI AMBAZO KANISA LIMESAHAU UPENDO WAKWANZA.KANISA LIMEPOA.WATU WAKO MOTO KISIASA ILA KIROHO WAMEPOA KABISA.NINYAKATI ZA YEYE ALIYE NASIKIO AYASIKIE HAYA AMBAYO ROHO ANAYAMBIA MAKANISA.HERI MWENYE SIKIO LAKUSIKIA SASA. NIMUDA WAKO WAKUJA KWENYE NENO LAUFUNUO IKIWA ULIMUULIZA MUNGU AKUONYESHE NIWAPI UENDE. SIMAMA KWAMIGUU YAKO NAUCHUKUE HATUA. 0763359745/0712583194

MFULULIZO WA MAFUNDISHO YA APOSTLE ALAM J. KAYENGELA KWENYE KONGAMANO LA SIKU NANE ARUSHA TANZANIA (TAREHE 5-12 MWAKA 2013)

SEHEMU YA PILI