Leoleoplus,com

NENO LA UFUNUO LA WIKI HII-Jinsi Neno la Ufunuo linavyo husika kuyafumbua macho yako






Luka 24;31 “Yakafumbuliwa macho yao wakamtambua; kisha akatoweka mbele yao”.
Macho yako yanapofumbuliwa ndipo unapomtambua Yesu. Macho yanayozungumzwa hapa siyo haya ya kawaida. Macho haya ya kawaida yamenajisiwa na vitu vingi kiasi kwamba Mungu hapendi kuyaruhusu yamwone (Ndio maana Mungu hujificha sana)

Mara nyingi watu waliofungwa na roho hii chafu ya kutaka kumwona Mungu kwa macho haya ya kawaida, ni wale waliotoka kwenye framilia ya Tomaso (wa kizazi kisichosadiki bila kuona).

NI MACHO GANI HASA YAFUMBULIWE KWANGU ILI NIMWONE MUNGU KILA MARA?

Efeso 1:18 “Macho ya mioyo yenu yatiwe nuru,………….” Ni macho ya moyo wangu. Yanapotiwa nuru na Neno la Ufunuo ndipo yanapofumbuka- Zaburi 119:130 “Kufafanusha maneno yako kwatia nuru, na kumfahamisha mjinga”
Sikuzote ifahamike ya kwamba Neno la Ufunuo ni lile lililofafanuliwa kiufunuo.

SABABU KUBWA INAYOSABABISHA MARA KWA MARA WEWE KUTOMWONA MUNGU

Hiyo sababu utaijua leo na kufumbuliwa macho yako. Si wengi wanaojua sababu inayosababisha mara kwa mara wasimwone Mungu.

Sababu hiyo ni kwamba, hujajua kumtazama Mungu kwa macho ya moyo. Wengi hawajui kama moyo una macho.

MACHO YA MOYO NI NINI?

Jibu ni rahisi- Macho ya moyo ni hisia takatifu maana yake unapokuwa kwenye maombi unamhisi Mungu kuwepo hapo ulipo saa hiyohiyo au muda huohuo. Hutahisi kuwa Mungu yuko mbali utahisi ukaribu wake kwako.

Macho ya moyoni ni fikra takatifu unayoiruhusu kumwona Mungu kwa kila jambo- Wakolosai 3:23 “Lolote mfanyalo, fanyeni kwa moyo, kama kwa Bwana, wala si kwa wanadamu”.
Maana yake hata unaposoma ujumbe huu hisia yako takatifu inaweza ikahisi uwepo wa Mungu akikufundisha.

Ninapotoa sadaka kwa ajili ya kusudi la Mungu na siyo kwa manufaa yangu tu kwa urahisi naelewa nafanya kwa Bwana. Kumbuka macho yako(macho ya moyo wako) hayatafumbuka bila Neno la Ufunuo.
            
            AMINA!!!!!

Comments

Popular posts from this blog

NENO LAUFUNUO LA LEO tazama Ayubu 8:7"Tena ujapokuwa huo mwanzo wako ulikuwa mdogo,lakini mwisho wako ungeongezeka sana"NENO LA UFUNUO LASIKU YAKO LEO. MUNGU ANAKUTAKA USIWE NAMAWAZO YA KUDHARAU MWANZO WAKOMDOGO. KWAMAANA TABIA YA MUNGU NIKWAMBA,YEYE HUWA HAUDHARAUMWANZO MDOGO. HATAKAMA NIMWANZO MDOGO YEYE HATAUDHARAU. "Mungu alianza na mwanadamu mmoja,leo hii wako mabilioni. Yesu alianza na wanafunzi kumi nawawili,leohii anawafuasi wengi hata hawana idadi maanawengine walishatangulia mbinguni. Historia yamakanisa mengi Africa na ulimwengu kwaujumla,yalianza namwazo mdogo sana lakini yamekuwa makubwa nayakushangaza."KILA MWANADAMU CHINI YAJUA ANAPITIA UZOEFU HUU WA KIPINDI CHAMWANZOMDOGO.LEO INABIDI UJIULIZE UKO KWENYEMWANZOMDOGO WAJAMBO GANI? JE UKO KWENYE MWANZOMDOGO WA KUANZISHA KAZI YAMUNGU? JE UKO KWENYEMWANZOMDOGO WANDOA? UKO KWENYEMWANZO WABIASHARA? UKO KWENYE MWANZO WA OFISI MPYA? UKO KWENYE MWANZO WAUCHUMBA? UKO KWENYE MWANZO WA AJIRA? UKO KWENYE MWANZO GANI? TAZAMA zekaria 4:10"maana ninani aliyeidharau siku yamambo madogo?.....OK. UNAONYWA! USIDHARAU MWANZO MDOGO ULIO NAO LEO. USIVUNJWE MOYO NAMWANZO MDOGO. USIKATISHWETAMAA NAMWANZO MDOGO.USIJIWAZIE VIBAYA KWASABABU YA MWANZO WAKO MDOGO. LEO,PIGA MOYO WAKO KONDE UCHANGAMKE MWISHO WAKO NIMZURI. MWISHO WAKO NIMKUBWA. POKEA NENO HILI LAUFUNUO ALILO KUTUMIA MUNGU SIKU YALEO.JITAHIDI UJE KANISANI UPATE MAELEKEZO ZAIDI. HUDUMA YA NENO LAUFUNUO CHINI YA MWANGALIZI MKUU MWL NA MTUME ARAM J.KAYENGELA IMEFANYIKA BARAKA SANA YAKIROHO NAKIMWILI KWAWOTE WALIO FANIKIWA KUJIUNGA RASMI. NIHUDUMA YAKIROHO YENYE UHUISHO MPYA KATIKA SIKU HIZI ZA HATALI AMBAZO KANISA LIMESAHAU UPENDO WAKWANZA.KANISA LIMEPOA.WATU WAKO MOTO KISIASA ILA KIROHO WAMEPOA KABISA.NINYAKATI ZA YEYE ALIYE NASIKIO AYASIKIE HAYA AMBAYO ROHO ANAYAMBIA MAKANISA.HERI MWENYE SIKIO LAKUSIKIA SASA. NIMUDA WAKO WAKUJA KWENYE NENO LAUFUNUO IKIWA ULIMUULIZA MUNGU AKUONYESHE NIWAPI UENDE. SIMAMA KWAMIGUU YAKO NAUCHUKUE HATUA. 0763359745/0712583194

MFULULIZO WA MAFUNDISHO YA APOSTLE ALAM J. KAYENGELA KWENYE KONGAMANO LA SIKU NANE ARUSHA TANZANIA (TAREHE 5-12 MWAKA 2013)

SEHEMU YA PILI