Leoleoplus,com

MFULULIZO WA MAFUNDISHO YA APOSTLE ALAM J. KAYENGELA KWENYE KONGAMANO LA SIKU NANE ARUSHA TANZANIA (TAREHE 5-12 MWAKA 2013)


SIKU YA 8:                                          
·         NAMNA YA KUPOKEA USHINDI WA MUNGU DHIDI YA MIUNGU.
-          Hii inamaanisha namna ya kupokea mbinu za kushinda miungu.

-          Misingi 4 ya vyanzo vya nguvu za Mungu inayokufanya upate NGUVU YA MUNGU ya kushinda miungu migeni ya kipepo.
·         Msingi wa kwanza: AMUA KUWA SADAKA
Unapofikia maamuzi haya ya kuwa sadaka ya Mungu siyo rahisi hatakidogo kushindwa na miungu.

·         Kumbuka  - Isaka alikuwa sadaka iliyotolewa kwa Mungu – Mwz 22:1 – 2. Ukubwani mwake, shetani alijaribu kumuangamiza kwa njaa kali – Mwz 26:1-5, Isaka alipitia msukosuko kwenye ndoa – Mwz 26:6-11 - bado Isaka alidhulumiwa visima zaidi ya viwili – Mst 18 – 23. Hayo yote ikiwa ni pamoja nayeye kucheleweshewa mtoto (uzao – Mwz 25:21) lakini pamoja na hayo yote aliibuka msindi na akawa mkuu – Mwz26:12-14 sadaka huwa haishindwi na miungu kamwe – Isaka alikuwa sadaka. Sadaka ya Mungu aliye hai.

·         Kumbuka – Samweli alikuwa sadaka ya Mungu – 1 Samweli 1:11 na Mst 24. Alizaliwa katika kipindi ambacho miungu ilikuwa imeharibu kabisa hali ya hewa ya kiroho – Neno  la Bwana la ufunuo lilikuwa adimu – 3:1 (b) ni wakati huo ndo miungu ilikuwa imeshika kasi kuendesha oparesheni za hapa na pale mpaka sanduku la Bwana likawa limechukuliwa – 1 Samweli 5:1-2. Samweli ukubwani mwake alipitia changamoto nyingi mpaka za kuchaniwa nguo – 1 Samweli 15:27 lakini hata hivyo hakushindwa. Adui si mara moja waliazimia mabaya kwa Samweli 19:18 – 24. Mpaka walisalimu amri kwa sababu Samweli alikuwa sadaka ya Mungu – Sadaka haishindwi.

·         Kumbuka Yesu Kristo alikuwa sadaka -Yoh 3:16 alianza kuviziwa na miungu iliyokuwa nyuma ya Herode akiwa bado mdogo tu wa miaka miwili – Math 2:13-18 miungu ya nyikani uso kwa uso ilipambana na Bwana Yesu bila mafanikio – Math 4:1-11, kwa sababu yeye alikuwa sadaka. Aliviziwa sana ili angalau aweze kukamatwa hata kwa maneno yake – Luka 20:20, ikashindikana. Kwa sababu sadaka haishindwi, mwisho Yesu Kristo aliibuka mshindi na akakiri hivyo – nimeshinda ulimwengu – Yoh 16:33 (b) hakushindwa. Alishinda.

·         Kumbuka pointi hii – ukiamua kuwa sadaka ya Mungu unapata neema ya kupakwa mafuta ya tofauti – ndivyo  Mungu anavyosema kwenye Zaburi 45:7, Sauli alipakwa mafuta ya chupa – 1 Samweli 10:1 – lakini Daudi alipakwa mafuta ya Pembe - 1 Samweli 16:13. Pembe inawakilisha nini? Ukisoma katika ufunuo 17:12 pembe ni ufalme au mamlaka yenye nguvu.

·         Msingi wa pili: ONGEZA USIKIVU WAKO WA KIROHO NA UWE MTU WA KUTULIA – ndipo utaweza kuishinda miungu. Miungu hautaishinda kwa maombi tu, “Hapana” msingi huu wa pili wa maisha ya kiroho, uwe ndo msingi wa maisha yako ya kila siku kuanzia leo. Katika Mwz 1:1-



2 Mungu alipoona matatizo ya ukiwa, utupu na giza, hakukurupuka kufanya chochote isipokuwa “ALITULIA KWANZA” baada ya kutulia alijua kipi aanze nacho, na kwa namna gani.

·         Siku ya kwanza – AkawekaNuru – Mst 3-5
·         Siku ya pili – Akaweka Anga (Mbingu) Mst 6-8
·         Siku ya tatu – Akaweka Nchi na bahari – Mst 9-13
·         Siku ya nne – Akaweka Mianga ya majira na nyakati pamoja na nyota – Mst 14-19
·         Siku ya tano – Akaweka Viumbe vya baharini na ndege wa angani – Mst 20 – 23
·         Siku ya sita – Akaweka Wanyama wa kila aina na mwanadamu – Mst 24 -31
·         Siku ya saba – Akastarehe bila kufanya chochote – Mwz 2:1 – Maana yake usifanye kazi kama roboti Pumzika.

·         Kutulia ni tabia ya Mungu inayokufanya uwe na mwelekeo wa kufanya vitu sahihi vilivyo katika mpangilio sahihi.
·         Mfano – Nini kingetokea kama Mungu angeumba samaki siku ya pili? Kwa maana bahari haikuwepo bado, nini kingetokea kama angeumba mwanadamu kabla ya Nchi? Maana yake angeishi baharini.
·         Usipokuwa na muda wa kutulia mbele za Mungu, kimawazo, kishughuli n.k. lazima miungu itakuchanganya tu, kwa sababu hautakuwa na mwelekeo. Kitu cha kufanya kesho utakifanya leo, cha leo utakifanya kesho – mahali pa kuweka viatu utaweka mswaki, mahali pa mswaki utaweka soksi, mahali pa soksi utaweka Biblia, mahali pa biblia utaweka nguo n.k. Ukitaka kuvaa kiatu, utakitafuta kwanza, kudhihirisha ujinga ulio nao wa kuweka vitu kwa mpangilio. Kwa namna hiyo miungu huwezi kuishinda kwa sababu huna mpangilio wala mwelekeo – umekuwa mtu wa kubebanisha mambo ovyo.
·         Madhara ya kukosa utulivu hata hayawezi kuvumilika – kwanza  hutajua uanze na lipi na umalize na lipi – zaidi ni kwamba unaandamwa na roho ya kuchelewa au kuchelewesha mambo, utakuwa mtu wa kuzunguka kila mara kwenye uwanja wa kutafuta vitu ambavyo umesahau ulipoviweka. Na utakuwa mtu wa kuanza upya kila mara kwa sababu unafanya vitu kabla ya wakati au kwa kuchelewa.
·         Msingi wa tatu – KUBALI MAPENZI YAKO YAVUNJIKE YA MUNGU YASIMAME – huo ndio ulikuwa moyo wa Daudi – Mungu akapendezwa  - Matendo 13:22 kwa sababu hiyo, Daudi akaishinda miungu – 1 Samweli 17:42-43. Fika hatua mambo yako yaharibike ya Mungu uyafanikishe.

·         Msingi wa nne – JINYENYEKESHE ILI UWE NA ROHO ZA MIUNGU WATAKATIFU NDANI YAKO.

-          Unakumbuka Danieli – kwa sababu ya unyenyekevu, ndani yake ziliachiliwa roho za miungu watakatatifu toka kwa Mungu – Danieli 5:11 – hizo siyo roho za mapepo, bali ni Roho 7 za Mungu – Ufunuo 5:6, hizi Roho 7 za Mungu ndo zile zimeorodheshwa kwenye Isaya 11:2.
-          Kuwa na Roho za miungu watakatifu ndani yako ni jinsi gani unajitahidi kutafuta tabia hizo 7 za Mungu ili ziwe maishani mwako.
-          Ukishakuwa na Roho za miungu watakatifu ndani yako, ndipo unakuwa mungu mdogo chini ya jua – 1 Samweli 4:8 – walitenda kama miungu. Ndipo Neno la Yoh 10:34 – 35 linatimia kwako “NDINYI MIUNGU”
                       
·         MAELEKEZO
-          Tafuta nafasi ya kufanya maombi ya kumwambia Roho mtakatifu akusaidie na kukuweka kwenye misingi hiyo 4.



v  ONYO!!!
Umekatazwa kutoa copy ujumbe ulioko kwenye karatasi hii ili kumpa mwingine,isipokuwa umeruhusiwa kumchukulia rafiki yako karatasi yake mwenyewe. Itakuwa dhambi ya makusudi ya kutokutii usipo zingatia onyo hili.

                                      AMINA!!!!.

Comments

Popular posts from this blog

NENO LAUFUNUO LA LEO tazama Ayubu 8:7"Tena ujapokuwa huo mwanzo wako ulikuwa mdogo,lakini mwisho wako ungeongezeka sana"NENO LA UFUNUO LASIKU YAKO LEO. MUNGU ANAKUTAKA USIWE NAMAWAZO YA KUDHARAU MWANZO WAKOMDOGO. KWAMAANA TABIA YA MUNGU NIKWAMBA,YEYE HUWA HAUDHARAUMWANZO MDOGO. HATAKAMA NIMWANZO MDOGO YEYE HATAUDHARAU. "Mungu alianza na mwanadamu mmoja,leo hii wako mabilioni. Yesu alianza na wanafunzi kumi nawawili,leohii anawafuasi wengi hata hawana idadi maanawengine walishatangulia mbinguni. Historia yamakanisa mengi Africa na ulimwengu kwaujumla,yalianza namwazo mdogo sana lakini yamekuwa makubwa nayakushangaza."KILA MWANADAMU CHINI YAJUA ANAPITIA UZOEFU HUU WA KIPINDI CHAMWANZOMDOGO.LEO INABIDI UJIULIZE UKO KWENYEMWANZOMDOGO WAJAMBO GANI? JE UKO KWENYE MWANZOMDOGO WA KUANZISHA KAZI YAMUNGU? JE UKO KWENYEMWANZOMDOGO WANDOA? UKO KWENYEMWANZO WABIASHARA? UKO KWENYE MWANZO WA OFISI MPYA? UKO KWENYE MWANZO WAUCHUMBA? UKO KWENYE MWANZO WA AJIRA? UKO KWENYE MWANZO GANI? TAZAMA zekaria 4:10"maana ninani aliyeidharau siku yamambo madogo?.....OK. UNAONYWA! USIDHARAU MWANZO MDOGO ULIO NAO LEO. USIVUNJWE MOYO NAMWANZO MDOGO. USIKATISHWETAMAA NAMWANZO MDOGO.USIJIWAZIE VIBAYA KWASABABU YA MWANZO WAKO MDOGO. LEO,PIGA MOYO WAKO KONDE UCHANGAMKE MWISHO WAKO NIMZURI. MWISHO WAKO NIMKUBWA. POKEA NENO HILI LAUFUNUO ALILO KUTUMIA MUNGU SIKU YALEO.JITAHIDI UJE KANISANI UPATE MAELEKEZO ZAIDI. HUDUMA YA NENO LAUFUNUO CHINI YA MWANGALIZI MKUU MWL NA MTUME ARAM J.KAYENGELA IMEFANYIKA BARAKA SANA YAKIROHO NAKIMWILI KWAWOTE WALIO FANIKIWA KUJIUNGA RASMI. NIHUDUMA YAKIROHO YENYE UHUISHO MPYA KATIKA SIKU HIZI ZA HATALI AMBAZO KANISA LIMESAHAU UPENDO WAKWANZA.KANISA LIMEPOA.WATU WAKO MOTO KISIASA ILA KIROHO WAMEPOA KABISA.NINYAKATI ZA YEYE ALIYE NASIKIO AYASIKIE HAYA AMBAYO ROHO ANAYAMBIA MAKANISA.HERI MWENYE SIKIO LAKUSIKIA SASA. NIMUDA WAKO WAKUJA KWENYE NENO LAUFUNUO IKIWA ULIMUULIZA MUNGU AKUONYESHE NIWAPI UENDE. SIMAMA KWAMIGUU YAKO NAUCHUKUE HATUA. 0763359745/0712583194

MFULULIZO WA MAFUNDISHO YA APOSTLE ALAM J. KAYENGELA KWENYE KONGAMANO LA SIKU NANE ARUSHA TANZANIA (TAREHE 5-12 MWAKA 2013)

SEHEMU YA PILI