Leoleoplus,com

MFULULIZO WA MAFUNDISHO YA APOSTLE ALAM J. KAYENGELA KWENYE KONGAMANO LA SIKU NANE ARUSHA TANZANIA (TAREHE 5-12 MWAKA 2013)


SIKU YA 5:                             
·         BAADHI YA AINA ZA MIUNGU YA WAFILISTI NA MIJI YA MADHABAHU ZAO.
1.    Dagoni – tazama, katika Waamuzi 16:23 – Dagoni alikuwa Mungu wa Wafilisti. Ni moja ya miungu iliyohusika katika harakati za kumkamata Samsoni – Waamuzi 16:1-31 Hata sasa ziko kazini hizo roho.

2.    Maashtorethi – 1 Samweli 31:8 – 13 – Maashtorethi ni miungu ya Wafilisti iliyoongoza operesheni za kummaliza Mfalme Sauli. Zinafanya hivyo hata leo.

3.    Beth – shan – Samweli 31:8-13 – Beth – Shan ni mungu wa Wafilisti anayeendesha shughuli za kujenga kuta. Ndiye anayejenga kuta hata nyakati zetu hizi.Kuta za kiroho

4.       Baal – Zebuhu – 2 Falme 1:2 – Baal – Zebubu ni Mungu wa kigeni wa Wafilist anayetenda kazi kwa ushirika wa karibu na Abadoni au Apolioni malaika wa kuzimu – Ufunuo 9:11 Baal – Zebubu kwa ushirika wa pamoja na Apolioni zilikuwa roho zilizoweza kuwavuta hata Wafalme kwenda kwa waganga wa kienyeji. Baal – Zebubu katika Agano jipya alitambulika kama – beel zebuli mkuu wa mapepo – Math 12:22 – 24.

5.       Baal – peori – Hesabu 25:1-3 baal – peori ni mungu wa wafilisti aliyeongoza harakati za kuwaunganisha wana wa Israeli na mtandao wa giza kwa njia ya uzinzi. Alitumia kizazi cha Moabu kutokana na historia ya chimbuko la Moabu lilivyokuwa – Mwz 19:30-38. Na ndicho anachokifanya leo.

6.       Baal – 1 Falme 18:25 – 26 – baal ni mungu wa wafilisti aliyemfanya Yezebeli kuwa Malkia wake katika ulimwengu wa giza – 1 Falme 19 : 1 – 2 upako wa kishetani wa Yezebeli, ulitiririka kutokakwa Malkia wa baharini na Malkia wa Pwani. Baal ndiye alikuwa nembo kuu ya miungu yote ya wafilisti.

·         Roho za miungu hii bado zinatenda kazi hata sasa, lakini kwa mchepuo wa tofauti. Bila neno la ufunuo siyorahisi kugundua.

·         MIJI 5 YA WAFILISTI – YOSHUA 13:2-3
1.       Gaza
2.       Ashdodi
3.       Ashkeloni
4.       Gathi
5.       Ekroni



Nguvu za uharibifu wa kipepo zilikuwa zinatokea katika miji hii. Mawimbi ya giza yalirushwa toka katika miji hii. Kulikuwa na nguvu ya pamoja iliyotoka kwenye muungano wa miji hii katika ulimwengu waroho. Ni vema kujua, nguvu unayopambana nayo inatoka katika mji gani/nchi gani.

·         Viongozi waliopewa upako wa kutawala miji hiyo 5.
Kidemokrasia au kisheria hata kisiasa – waliitwawakuu wa miji, na mashehe watano wa wafilisti – Yoshua 13:3 neno Mashehe, katika nyakati zetu lisitafsiriwe vibaya, kwani tokea mwanzo lilimaanisha kama kiongozi wa mji aliyepewa heshima. Kwani hata Nehemia mtumishi wa Mungu aliye hai  - alilitumia kwenda kuwaambia viongozi Fulani ili wafanikishe kazi ya Mungu wa kweli – Neh 4:14. Viongozi wa miji hiyo 5 katika ulimwengu wa roho walitambulika kama wakuu wa giza wanaotenda kazi kwa mkusanyiko wa nguvu ya pamoja. Wana harakati wakuu wa milango ya kuzimu, pia walikuwa wakuu wa mila na desturi. Walihusika kwa kila tukio lililohusiana na watumishi wa Mungu katika kilele cha vizuizi na upinzani.

·         Kila miji unayoiona katika bara la Africa miungu imeweka wakuu wa hiyo miji katika namna ya usiri mkubwa, ilikuachilia nguvu za giza katika Nyanja tofauti tofauti.

·         Kwa sababu hiyo, kuna ulazima wa kuzingatia ukweli kwamba, maombi yako yafuatane na mji uliopo. Yaani kuomba kwako kuungane na hekima ya kushughulikia ulimwengu waroho wa mji wako. Usisahau hilo.

MAELEKEZO
1.       Dagoni
2.       Maashtoreth
3.       Beth – shan\baal – zebubu
4.       Baal – peori
5.       Baal
·         Jifunze kufanya maombi kwa kushughulikia roho za miungu hii zinazopunguza spidi za maendeleo yako kiroho na kimwili. Piga miungu hiyo katika ulimwengu wako wa maombi, mpaka inaposalimu amri, ifurumishie mawe ya moto mpaka inapotoroka.

MAOMBI
1.       Damu ya yesu kristo, peleka kizaazaa kwenye miji mitano ya kiroho iliyoungana kwa ajili ya kuunda nguvu ya panoja ya kunimaliza – katika jina la Yesu kristo.

2.       Roho mtakatifu – sababisha mahangaiko na vifo vya ghafla kwa wakuu wa giza watano walioungana kwaajili ya kukomesha na kuimaliza hatma yangu - katika jina la Yesu kristo.

3.       Mungu Baba Mungu Mwana Mungu Roho mtakatifu ifungue nafsi yangu isiendelee kushikiliwa na miungu ya kigeni kwa namna yoyote nisiyoijua - katika jina la Yesu kristo.

4.       Moto wa Mungu vunja pingu za miungu ya wafilisti kwenye mikono na miguu yangu - katika jina la Yesu kristo.

5.       Miungu mnaoleta milango ya kuzimu nyumbani kwangu mpigwe mweleka na nguvu za moto ulao mnikimbie mara moja - katika jina la Yesu kristo.


v  ONYO!!!
Umekatazwa kutoa copy ujumbe ulioko kwenye karatasi hii ili kumpa mwingine,isipokuwa umeruhusiwa kumchukulia rafiki yako karatasi yake mwenyewe. Itakuwa dhambi ya makusudi ya kutokutii usipo zingatia onyo hili.

AMINA!!!!.

Comments

Popular posts from this blog

NENO LAUFUNUO LA LEO tazama Ayubu 8:7"Tena ujapokuwa huo mwanzo wako ulikuwa mdogo,lakini mwisho wako ungeongezeka sana"NENO LA UFUNUO LASIKU YAKO LEO. MUNGU ANAKUTAKA USIWE NAMAWAZO YA KUDHARAU MWANZO WAKOMDOGO. KWAMAANA TABIA YA MUNGU NIKWAMBA,YEYE HUWA HAUDHARAUMWANZO MDOGO. HATAKAMA NIMWANZO MDOGO YEYE HATAUDHARAU. "Mungu alianza na mwanadamu mmoja,leo hii wako mabilioni. Yesu alianza na wanafunzi kumi nawawili,leohii anawafuasi wengi hata hawana idadi maanawengine walishatangulia mbinguni. Historia yamakanisa mengi Africa na ulimwengu kwaujumla,yalianza namwazo mdogo sana lakini yamekuwa makubwa nayakushangaza."KILA MWANADAMU CHINI YAJUA ANAPITIA UZOEFU HUU WA KIPINDI CHAMWANZOMDOGO.LEO INABIDI UJIULIZE UKO KWENYEMWANZOMDOGO WAJAMBO GANI? JE UKO KWENYE MWANZOMDOGO WA KUANZISHA KAZI YAMUNGU? JE UKO KWENYEMWANZOMDOGO WANDOA? UKO KWENYEMWANZO WABIASHARA? UKO KWENYE MWANZO WA OFISI MPYA? UKO KWENYE MWANZO WAUCHUMBA? UKO KWENYE MWANZO WA AJIRA? UKO KWENYE MWANZO GANI? TAZAMA zekaria 4:10"maana ninani aliyeidharau siku yamambo madogo?.....OK. UNAONYWA! USIDHARAU MWANZO MDOGO ULIO NAO LEO. USIVUNJWE MOYO NAMWANZO MDOGO. USIKATISHWETAMAA NAMWANZO MDOGO.USIJIWAZIE VIBAYA KWASABABU YA MWANZO WAKO MDOGO. LEO,PIGA MOYO WAKO KONDE UCHANGAMKE MWISHO WAKO NIMZURI. MWISHO WAKO NIMKUBWA. POKEA NENO HILI LAUFUNUO ALILO KUTUMIA MUNGU SIKU YALEO.JITAHIDI UJE KANISANI UPATE MAELEKEZO ZAIDI. HUDUMA YA NENO LAUFUNUO CHINI YA MWANGALIZI MKUU MWL NA MTUME ARAM J.KAYENGELA IMEFANYIKA BARAKA SANA YAKIROHO NAKIMWILI KWAWOTE WALIO FANIKIWA KUJIUNGA RASMI. NIHUDUMA YAKIROHO YENYE UHUISHO MPYA KATIKA SIKU HIZI ZA HATALI AMBAZO KANISA LIMESAHAU UPENDO WAKWANZA.KANISA LIMEPOA.WATU WAKO MOTO KISIASA ILA KIROHO WAMEPOA KABISA.NINYAKATI ZA YEYE ALIYE NASIKIO AYASIKIE HAYA AMBAYO ROHO ANAYAMBIA MAKANISA.HERI MWENYE SIKIO LAKUSIKIA SASA. NIMUDA WAKO WAKUJA KWENYE NENO LAUFUNUO IKIWA ULIMUULIZA MUNGU AKUONYESHE NIWAPI UENDE. SIMAMA KWAMIGUU YAKO NAUCHUKUE HATUA. 0763359745/0712583194

MFULULIZO WA MAFUNDISHO YA APOSTLE ALAM J. KAYENGELA KWENYE KONGAMANO LA SIKU NANE ARUSHA TANZANIA (TAREHE 5-12 MWAKA 2013)

KUJUA KUTEMBEA NA MUNGU NIPAMOJA NAKUJUA KUSOMA ALAMA ZA NYAKATI KATIKA ROHO