Leoleoplus,com

MFULULIZO WA MAFUNDISHO YA APOSTLE ALAM J. KAYENGELA KWENYE KONGAMANO LA SIKU NANE ARUSHA TANZANIA (TAREHE 5-12 MWAKA 2013)


SIKU YA 6:                             
·         MIUNGU NA MAKABILA YA VIZAZI VILE.
Miungu ilisonga mbele kwa makusudi makuu kwenye mzunguko wa ulimwengu wa makabila.

·         Baadhi ya miungu na harakati zake juu ya makabila 2Falme 23:13.
1.       Ashtoreshi – alikuwa mungu mke wa kabila la wasidoni, kama inavyoonekana katika 1 Walue 11:33. Ashtoreshi ni kirefu cha “Ashera” ambaye pia aliaminiwa kuwa ni mungu anayefanikisha uzazi wa kila kitu.

2.       Kemoshi – alikuwa mungu wa wamoabi – mungu kemoshi na baal – peori ni miungu iliyowatesa sana kabila la moabi hata kwa kuwafanya kuwa waasherati na wazinzi – Hesabu 25:1 – 3.

3.       Milkomu au moleki – alikuwa mungu wa Amoni. Moleki alilitawala na kulikandamiza kabila la waamoni. Mungu moleki ndiye aliyelifanya kabila la waamoni kuamini kwamba, wakitoa sadaka ya kafara ya watoto watafanikiwa na kuwa karibu na mungu – Lawi 20:1 – 5 na 2Falme 17:17 ndiye anayeongoza ibada za kafara za watoto mpaka leo, na kafara za mimba changa. Sulemani alipomuoa mke wa Amoni bila kujua miungu ya chimbuko lake, ghafla nafsi yake ilinaswa katika ulimwengu wa giza na akaanza kujenga madhabahu kwa ajili ya mungu Moleki. Na kuanzia hapo miungu 4 ilianza kummiliki – 1Falme 11:5 -7.

·         Unaposoma 1Falme 11:5-8
-          Unagundua kuwa, nafsi ya Mfalme Sulemani ilifungwa pingu na miungu 4.
1.       Ashtoreshi – mungu mke wa wasidoni
2.       Milkomu au moleki – mungu wa Waamoni
3.       Kemoshi – mungu wa Wamoabu
4.       Baal – miungu ya Wafilisti ambayo aliitolea sadaka.

·         Undani wa makabila ya vizazi vile
-          Miungu hushughulika sana na vichwa vya makaabila au wakuu wa makabila – mfano: Mwa 49:3-4 Rubeni alipozini na mke wa baba yake – aliharibu hatima ya kizazi chake – Kutoka 6;14 1Nyakati 5:1-3 watoto wake wanne yaani Hanoki, na Palu na Hersoni na Karmi – Baraka zao zilienda kwa Yusufu – 1 Nyakati 5:1. Huwezi ukajua leo kichwa cha kabila lako au mkuu wa kabila lako alifanya nini na Mungu au miungu, lakini unaweza kusoma alama kwa kuona matokeo ya maisha uliyonayo.




·         Pingu za kabila
-          Chunguza vizuri katika Amosi 1:6-8 – Hapo unaona kabila zima limepigwa pingu na kufungwa kisha kutiwa katika mikono ya Edomu (roho ya kuhangaika na kufa vibaya) nguvu hiyo ya kulifunga kabila zima ilitoka kwenye kati ya miji ile 5 ya wakuu wa Wafilisti (wakuu wa giza) waliokuwa wanatawala miji mitano ya wafilist. Kwa hiyo kabila zima lilifungwa kwa upako wa giza ulioachiliwa kutoka kwenye miji 4 ya wakuu wa giza – yaani, Gaza, Ashdodi na Ashkeloni pamoja na Ekroni.

-          Miungu iliweza kulifunga kabila zima. Je! Iliwezekanaje kukamata kabila lote na kulifunga? Kwa kupitia mtu mmoja (mkuu wa kabila) miungu ikalifunga kabila.

·         Viapo vya kabila
Unaposoma vizuri katika Habakuki – 3:9 unaona wazi kwamba kuna viapo vya kabila au makabila. Sasa hatima yako inategemea kiapo alichofanya mkuu wa kabila lako. Aliapa kumtumikia Mungu wa kweli au miungu mingine? Katika bara la Africa makabila mengi na koo nyingi wakuu wao waliapa kwa makusudi kujitoa nafsi zao kwa miungu ya kipepo.

·         Miungu na makabila ya vizazi vile, ni jambo muhimu linalopaswa kuhamasisha fahamu zako binafsi kugundua ukweli kwamba upo umuhimu katika kizazi chako leo kujitahidi kujua namna ya kutumia nguvu ya mungu wa kweli, dhidi ya miungu ambayo kwa siri kubwa imefanikiwa kupoozesha kanisa hasa kupitia makabila.

·         MAOMBI
1.       Ee Mungu wa mipango mema juu yangu, nakupa sifa na shukurani kwa kuwa umenifanya kuwa wa uzao wa Ibrahim na wa kabila la simba wa Yuda kwa kupitia mpendwa Yesu Kristo. Kwa sababu hiyo ninaikiri Damu ya Yesu Kristo juu ya kabila langu la zamani ambalo miungu yake haikomi kunifuatilia. Miungu ya kabila langu la zamani nilipokuwa sijaokoka nawapigia makofi ya kuwachanganya na kuwapotosha milele (piga sasa kwa nguvu unapoendelea na maombi haya). Pingu za miungu ya giza mlionifunga kupitia kabila langu moto ukukate kama uzi unavyokatwa na moto. Pingu za mapepo kutoka kwenye chimbuko langu la kuzaliwa katika ukoo na kabila langu niache mara moja, pigwa na malaika wa vita – Katika Jina la Yesu Kristo.

Katika jina la Yesu Kristo, nasimama kinyume na viapo vya uharibifu walivyofanya wakuu wa kabila langu kwa miungu ya kishetani – Katika Jina la Yesu Kristo.
 Ninakataakuathiriwa na viapo walivyofanya wakuu wa ukoo wangu, wakuu wa kabila langu, wakuu wa mji wangu, wakuu wa kitongoji changu – kwa Jna la Yesu Kristo.

MAELEKEZO
1.       Yale ambayo wazee wako hawakufanya kwa Mungu wa kweli – wewe yafanye kwa bidii, ili usiweze kurudi kwenye pingu za miungu ya kipepo.

2.       Usisahau katika kipengele hiki unapoomba,omba ukiwa unapiga makofi kwa nguvu utaona kila wakati upako waRoho mtakatifu ukiisumbua miungu inayokusumbua.

v  ONYO!!!
Umekatazwa kutoa copy ujumbe ulioko kwenye karatasi hii ili kumpa mwingine,isipokuwa umeruhusiwa kumchukulia rafiki yako karatasi yake mwenyewe. Itakuwa dhambi ya makusudi ya kutokutii usipo zingatia onyo hili.

                                              AMINA!!!!.

Comments

Popular posts from this blog

NENO LAUFUNUO LA LEO tazama Ayubu 8:7"Tena ujapokuwa huo mwanzo wako ulikuwa mdogo,lakini mwisho wako ungeongezeka sana"NENO LA UFUNUO LASIKU YAKO LEO. MUNGU ANAKUTAKA USIWE NAMAWAZO YA KUDHARAU MWANZO WAKOMDOGO. KWAMAANA TABIA YA MUNGU NIKWAMBA,YEYE HUWA HAUDHARAUMWANZO MDOGO. HATAKAMA NIMWANZO MDOGO YEYE HATAUDHARAU. "Mungu alianza na mwanadamu mmoja,leo hii wako mabilioni. Yesu alianza na wanafunzi kumi nawawili,leohii anawafuasi wengi hata hawana idadi maanawengine walishatangulia mbinguni. Historia yamakanisa mengi Africa na ulimwengu kwaujumla,yalianza namwazo mdogo sana lakini yamekuwa makubwa nayakushangaza."KILA MWANADAMU CHINI YAJUA ANAPITIA UZOEFU HUU WA KIPINDI CHAMWANZOMDOGO.LEO INABIDI UJIULIZE UKO KWENYEMWANZOMDOGO WAJAMBO GANI? JE UKO KWENYE MWANZOMDOGO WA KUANZISHA KAZI YAMUNGU? JE UKO KWENYEMWANZOMDOGO WANDOA? UKO KWENYEMWANZO WABIASHARA? UKO KWENYE MWANZO WA OFISI MPYA? UKO KWENYE MWANZO WAUCHUMBA? UKO KWENYE MWANZO WA AJIRA? UKO KWENYE MWANZO GANI? TAZAMA zekaria 4:10"maana ninani aliyeidharau siku yamambo madogo?.....OK. UNAONYWA! USIDHARAU MWANZO MDOGO ULIO NAO LEO. USIVUNJWE MOYO NAMWANZO MDOGO. USIKATISHWETAMAA NAMWANZO MDOGO.USIJIWAZIE VIBAYA KWASABABU YA MWANZO WAKO MDOGO. LEO,PIGA MOYO WAKO KONDE UCHANGAMKE MWISHO WAKO NIMZURI. MWISHO WAKO NIMKUBWA. POKEA NENO HILI LAUFUNUO ALILO KUTUMIA MUNGU SIKU YALEO.JITAHIDI UJE KANISANI UPATE MAELEKEZO ZAIDI. HUDUMA YA NENO LAUFUNUO CHINI YA MWANGALIZI MKUU MWL NA MTUME ARAM J.KAYENGELA IMEFANYIKA BARAKA SANA YAKIROHO NAKIMWILI KWAWOTE WALIO FANIKIWA KUJIUNGA RASMI. NIHUDUMA YAKIROHO YENYE UHUISHO MPYA KATIKA SIKU HIZI ZA HATALI AMBAZO KANISA LIMESAHAU UPENDO WAKWANZA.KANISA LIMEPOA.WATU WAKO MOTO KISIASA ILA KIROHO WAMEPOA KABISA.NINYAKATI ZA YEYE ALIYE NASIKIO AYASIKIE HAYA AMBAYO ROHO ANAYAMBIA MAKANISA.HERI MWENYE SIKIO LAKUSIKIA SASA. NIMUDA WAKO WAKUJA KWENYE NENO LAUFUNUO IKIWA ULIMUULIZA MUNGU AKUONYESHE NIWAPI UENDE. SIMAMA KWAMIGUU YAKO NAUCHUKUE HATUA. 0763359745/0712583194

MFULULIZO WA MAFUNDISHO YA APOSTLE ALAM J. KAYENGELA KWENYE KONGAMANO LA SIKU NANE ARUSHA TANZANIA (TAREHE 5-12 MWAKA 2013)

KUJUA KUTEMBEA NA MUNGU NIPAMOJA NAKUJUA KUSOMA ALAMA ZA NYAKATI KATIKA ROHO