Leoleoplus,com

MFULULIZO WA MAFUNDISHO YA APOSTLE ALAM J. KAYENGELA KWENYE KONGAMANO LA SIKU NANE ARUSHA TANZANIA (TAREHE 5-12 MWAKA 2013)


SIKU YA 7:                                          
·         KAZI ZA MIUNGU YA WAFILISTI.
1.    Kufuatilia na kuvizia watu maalumu waliokabidhiwa kitu maalumu na Mungu.
-          Hili linapaswa liwe onyo muhimu hasa kwa watu Fulani waliokabidhiwa jukumu maalumu na Mungu. Umuhimu wa jambo hili, hatuwezi kuuelewa kwa ukamilifu kwa akili zetu hizi za kibinadamu zilizojaa ubinadamu. Kufuatilia na kuvizia watu maalumu waliokabidhiwa kitu maalumu na Mungu ni moja ya vipaumbele vya shughuli za miungu ya wafilisti. Mfano Mfalme Sauli kwa mashimo makubwa mawili, miungu ilifanikiwa kummaliza.

1.    shimo la kukosa uvumilivu wa kiimani – 1 Samwel 13:8 – 14 – shimo hilo linatafsiriwa
        kama upambavu mbeleza Mungu – Mst 13 matokeo yake ni kunyang’anywa kile
      ulichokuwa umepewa na atapewa mwingine Mst 14.

2.    Shimo la kukosa utii wa uaminifu – 1 Sam 15:1- 23 katika ulimwengu war oho shimo hili linatafsiriwa kama –  uovu – Mst 19 na uchawi – Mst 23 – ndipo hali hiiinakupofusha macho usione kosa pale unapokosea bali ujihesabie haki – Mst 19 – 20. Aliambiwa “Umekosea” Akajibu “Hapana nimetii” Hakuliona kosa.

Mashimo haya mawili ya milango ya kuzimu ya miungu ya wafilisti yalifanyika kuwa pingu na tanzi ya kummaliza Mpakwa mafuta maalumu wa Mungu – 1 Samweli 10:1. Wafilisti wakiwa na uvuvio wa nguvu za miungu, wakamfuatilia sana Sauli kwa umakini bila makosa, vita vikawa vikali sana  mpaka “WAKAMPATA” – 1 Samweli 31:1-3 Sauli alijiua kimwili lakini akiwa ameshakamatwa kwenye ulimwengu waroho – 1Sam 31:3-5 – Wafilisti baada ya kumpata Sauli wakafanya sherehe na kuitukuza miungu yao iliyofanikisha kukamatwa kwake – 1Samweli 31:8 – 10 – ukawa mwisho wa mtu huyo maalum.

·         Mfano wa pili – Samsoni mtu maalumu wa Mungu
-          Samsoni hakuwa mlokole wa kawaida hapa duniani bali alikuwa maalumu aliyekuwa na kitu maalumu. Umaalumu wake unaonekana kuanzia kwenye chimbuko lake la kuzaliwa – Waamuzi 13:1-25. Chimbuko la ukoo wake wa kikabila alikuwa wa ukoo wa Dani – Mst2. Alikuwa mnadhiri toka tumboni – maana yake alikuwa “Maalumu – Mst7”. Aliinuliwa na Mungu  ili awe mwamuzi wa Waisraeli. Akatumikia kusudi hilo yapata miaka ishirini -Waamuzi 16;31 (b).


Miungu ilikuwa mbioni kumfuatilia mtu huyu maalum wa Mungu kupitia Wafilisti – Waamuzi 16:2 kwa mara ya kwanza Samsoni akafaulu kukwepa – Mst3. Lakini haikuchukua muda tayari alikuwa amekamatwa Mst 21, ili kumfanya awe dhaifu zaidi kitu cha kwanza waling’oa macho yake – Mst 21. Hakukamatwa na Wafilisti pekee bali ilikuwa miungu hiyo, ikawa nilazima Wafilisti kuitolea sadaka ya shukrani miungu hiyo – Mst23- 24. Mungu Dagoni ndiye aliyeendesha oparesheni hiyo ya kukamatwa kwa Samsoni Mst 23. Usifanye mchezo na miungu unahitaji kuongeza umakini wa kujua namna ya kutumia nguvu ya Mungu dhidi ya miungu.

·         Mfano wa tatu ni Yesu Kristo – Japo alikuwa mtu maalum wa Mungu, kwa ukaribu sana alifuatiliwa na kuviziwa sana – Luka 20:21. Katika Agano jipya – Yesu alikuwa anaviziwa na nguvu tatu kubwa za miungu – Beelzlzebuli yaani Mkuu wa mapepo – Math 12:23 – 24 na Apolioni au Abadoni ambaye ni Malaika wa kuzimu- Ufunuo 9:11 pamoja na Mfalme wa uweza wa anga – Efeso 2: 1-3 Bwana Yesu alishinda miungu hii kwa jinsi alivyotembea na misingi 4 ya kiroho ambayo nitakuwa naifunua kesho kwa uwezo waRoho mtakatifu 1 Korinto 2:10.

2.Kufukia na kugombania mipenyo yako
- Hii ndiyo kazi ya miungu ya Wafilisti, inafanya juhudi ya hali ya juu ili kufukia na kugombania upenyo wako. Angalia mfano kwa Isaka – Mwz 26:15 – 22.
1. Wafilisti walinyang’anya kisima – Mwz 21:25
2. Wafilisti wakagombania kisima – Mwz 26:18 - 22
3. Wafilisti walifukia pia kisima – Mwz 26 : 15
Miungu ya Wafilisti ilimfuatilia Isaka kwa namna hiyo, hasa kwa upande wa uchumi – akawa ameishinda na akawa mkuu – Mwz 26:12 – 14 hakutaka kushindwa.

3.    Miungu inasababisha Mungu asikujibu kwa sauti ya wazi, kwa ndoto na urimu – 1Sam 28:6
a.       Sauti ya wazi ni nini? – ni ile sauti unayoweza kusikia hata kwa masikio haya ya kawaida – Matendo 13:2-3 n.k
b.      Sauti ya ndoto ni nini? – ni vile Mungu anavyoweza kuku ambia au kukuonyeshakitu ukiwa umelala usingizi mzito – Ayubu 33:14 – 15.
c.       Urimu ni nini? – Kutoka 28:15 – 30, Hesabu 27:21na 1Samweli 14:41 pia na Ezra 2:63 – kwa hiyo, urimu ni kitu kilichotumiwa na kuhani mkuu au kiongozi mkuu kwa ajili ya kutafuta jibu la hapana au ndiyo kwa Mungu –kwahiyo kuhani mkuu alipotumia urimu kwaajili yakupata jibu la hapana au ndiyo kwa Mungu alifanya nfano unavyoweza kuchukua sarafu mbili kabla ya kuzirusha juu kwa pamoja, unamwambia Mungu kwamba, ikiwa sarafu hizi zitaonyesha namba- jibu litakuwa ni NDIYO ikiwa zitaonyesha sura ya picha jibu litakuwa ni HAPANA ikiwa moja itaonyesha namba na nyingine sura ya picha – jibu litakuwa ni HAKUNA JIBU, kwa hiyo baada ya kutamka maneno kama hayo – kuhani huyo alirusha juu na kuangalia kile Mungu atamwambia. Hiyo ni moja ya njia kubwa ambayo Mungu aliitumia ili kumjibu mtu wake kwa ajili ya kuthibitisha jambo furani. Hicho ni kitu cha kawaida tu, kwa sababu ni kama vile tu, unavyoweza kumuomba Mungu aina ya MAOMBI YA ISHARA – Waamuzi 6:36-40 maombi haya ya ishara nimeyaelezea sana kwenye kile kitabu cha AINA 90 ZA MAOMBI.








4.    Kuondoa utukufu.
Unapookoka – Bwana Yesu anaruhusu utukufu wa Mungu kuja juu yako – Yohana 17:22 mara moja miungu huanza kukufuatilia ili kukuondolea huo utukufu. Unabaki mkavu bila uwepo na nguvu ya Mungu. Fuatilia vizuri katika 1 Samweli 3:1-21, 4:1-22 na 5:1-12. Mungu Dagoni wa Wafilisti aliongoza oparesheni yakuondoa utukufu wa Mungu wa Israeli kwa wana wa Israel. Ikabodi ina maa utukufu umeondoka. Baada ya  IKabodi kuondoka ndipo wana wa Israeli wakapigwa sana na Wafilisti.

5.    Kuandaa milango ya kuzimu
-          Katika Mathayo 16:18 Bwana Yesu alisema kwamba milango ya kuzimu haitalishinda kanisa lake. Kwa hiyo alionyesha wazi kwamba, kanisa linashindana sana na milango ya kuzimu. Miungu inaandaaje milango ya kuzimu? Tazama kwenye Waamuzi 16:5 wakuu watano wa Wafilisti walimuandaaDelila kama mlango wa kuzimu wakamkamata mtu maalumu wa Mungu – Samsoni. Miungu  kabla ya kukumaliza, inatafuta kwanza kujua asili ya nguvu zako ni nini? Asili ya nguvu za Samsoni ilikuwa kwenye nywele na hapo ndipo miungu ilienda kushughulikia. Milango ya kuzimu ambayo ndiyo mikono ya miungu ya Wafilisti kazi yake ni kukumaliza kwenye asili ya nguvu zako.

MAOMBI:
1.      Roho Mtakatifu naomba saa hii upigane na miungu yote iliyonizunguka katika ulimwengu waraho – Katika Jina la Yesu Kristo.

2.      Mawakala wa miungu mnaovizia uhai wangu mpigwe butwaa nakuchanganyikiwa kisha mfe - Katika Jina la Yesu Kristo.

3.      Roho mtakatifu piga moto kazi zote za miungu kwenye maisha yangu - Katika Jina la Yesu Kristo.

4.      Kila oparesheni kubwa na ndogo ambazo miungu wanafanya ili kunikamata na kunimaliza – Roho mtakatifu kataa pamoja na mimi - Katika Jina la Yesu Kristo.

5.      Roho mtakatifu ifiche sura yangu wala miungu haitaniona kwenye Darubini zao - Katika Jina la Yesu Kristo.
MAELEKEZO
1.      Rudi kule mwanzo wa somo hili, uchukue mfano wa Mfalme Sauli utajua kwanini miungu ilimmaliza – hivyo wewe uwe makini.


v  ONYO!!!
Umekatazwa kutoa copy ujumbe ulioko kwenye karatasi hii ili kumpa mwingine,isipokuwa umeruhusiwa kumchukulia rafiki yako karatasi yake mwenyewe. Itakuwa dhambi ya makusudi ya kutokutii usipo zingatia onyo hili.

                                      AMINA!!!!.

Comments

Popular posts from this blog

NENO LAUFUNUO LA LEO tazama Ayubu 8:7"Tena ujapokuwa huo mwanzo wako ulikuwa mdogo,lakini mwisho wako ungeongezeka sana"NENO LA UFUNUO LASIKU YAKO LEO. MUNGU ANAKUTAKA USIWE NAMAWAZO YA KUDHARAU MWANZO WAKOMDOGO. KWAMAANA TABIA YA MUNGU NIKWAMBA,YEYE HUWA HAUDHARAUMWANZO MDOGO. HATAKAMA NIMWANZO MDOGO YEYE HATAUDHARAU. "Mungu alianza na mwanadamu mmoja,leo hii wako mabilioni. Yesu alianza na wanafunzi kumi nawawili,leohii anawafuasi wengi hata hawana idadi maanawengine walishatangulia mbinguni. Historia yamakanisa mengi Africa na ulimwengu kwaujumla,yalianza namwazo mdogo sana lakini yamekuwa makubwa nayakushangaza."KILA MWANADAMU CHINI YAJUA ANAPITIA UZOEFU HUU WA KIPINDI CHAMWANZOMDOGO.LEO INABIDI UJIULIZE UKO KWENYEMWANZOMDOGO WAJAMBO GANI? JE UKO KWENYE MWANZOMDOGO WA KUANZISHA KAZI YAMUNGU? JE UKO KWENYEMWANZOMDOGO WANDOA? UKO KWENYEMWANZO WABIASHARA? UKO KWENYE MWANZO WA OFISI MPYA? UKO KWENYE MWANZO WAUCHUMBA? UKO KWENYE MWANZO WA AJIRA? UKO KWENYE MWANZO GANI? TAZAMA zekaria 4:10"maana ninani aliyeidharau siku yamambo madogo?.....OK. UNAONYWA! USIDHARAU MWANZO MDOGO ULIO NAO LEO. USIVUNJWE MOYO NAMWANZO MDOGO. USIKATISHWETAMAA NAMWANZO MDOGO.USIJIWAZIE VIBAYA KWASABABU YA MWANZO WAKO MDOGO. LEO,PIGA MOYO WAKO KONDE UCHANGAMKE MWISHO WAKO NIMZURI. MWISHO WAKO NIMKUBWA. POKEA NENO HILI LAUFUNUO ALILO KUTUMIA MUNGU SIKU YALEO.JITAHIDI UJE KANISANI UPATE MAELEKEZO ZAIDI. HUDUMA YA NENO LAUFUNUO CHINI YA MWANGALIZI MKUU MWL NA MTUME ARAM J.KAYENGELA IMEFANYIKA BARAKA SANA YAKIROHO NAKIMWILI KWAWOTE WALIO FANIKIWA KUJIUNGA RASMI. NIHUDUMA YAKIROHO YENYE UHUISHO MPYA KATIKA SIKU HIZI ZA HATALI AMBAZO KANISA LIMESAHAU UPENDO WAKWANZA.KANISA LIMEPOA.WATU WAKO MOTO KISIASA ILA KIROHO WAMEPOA KABISA.NINYAKATI ZA YEYE ALIYE NASIKIO AYASIKIE HAYA AMBAYO ROHO ANAYAMBIA MAKANISA.HERI MWENYE SIKIO LAKUSIKIA SASA. NIMUDA WAKO WAKUJA KWENYE NENO LAUFUNUO IKIWA ULIMUULIZA MUNGU AKUONYESHE NIWAPI UENDE. SIMAMA KWAMIGUU YAKO NAUCHUKUE HATUA. 0763359745/0712583194

MFULULIZO WA MAFUNDISHO YA APOSTLE ALAM J. KAYENGELA KWENYE KONGAMANO LA SIKU NANE ARUSHA TANZANIA (TAREHE 5-12 MWAKA 2013)

SEHEMU YA PILI