Leoleoplus,com

MFULULIZO WA MAFUNDISHO YA APOSTLE ALAM J. KAYENGELA KWENYE KONGAMANO LA SIKU NANE ARUSHA TANZANIA (TAREHE 5-12 MWAKA 2013)


SIKU YA 3:                             
·         KUFUATILIWA NA WAMILIKI AU MMILIKI WA MIUNGU NA JINSI YA KUMSHINDA.
Mmiliki wa miungu, ana cheo kikubwa sana katika ulimwengu waroho. Ni kwa sababu, chini yake anatumikiwa na majeshi mengi ya mapepo. Kimo cha chini anakuwa na wastani wa mapepo milioni 40. Yote yanatenda kazi kwa amri yake. Ana utisho usio wa kawaida katika ulimwengu wa kipepo.

·         Nabii Eliya baada ya kuua  manabii 450 wabaal  waliokuwa wanamilikiwa na Yezebeli,      mwanamke aliyekuwa mmiliki wa miungu – 1Falme 18:17 – 19, 22 na 36 – 40 mmiliki wa miungu huyu Yezebeli alitoa tangazo makini kumwambia mtumishi wa Mungu ajipange kwa ajili ya kupambana naye kesho – 1Falme 19:1 – 3. Kwa kujua kile ambacho kilikuwa ni hakika kingemtokea – baada ya taarifa hiyo, Eliya aliamua kukimbia. Akamkimbia Yezebeli.. ni siku chache tu, Nabii Eliya alikuwa amewaua Manabii 450 wa kipepo. Aliwashinda 450 akiwa peke yake lakini alimkimbia mmiliki wa miungu mmoja Yezebeli.

·         Mika asiyeokoka – mmiliki wa miungu kwa kudhamiria kabisa aliwafuatilia wana wa Dani kwa juhudi kubwa huku akipiga kelele – Waamuzi 18:11 – 31 kwa sababu nawao walikuwa wamiliki wa miungu wakaonekana kuwa wana nguvu kuliko yeye akawa ameshindwa kwani walimtahadharisha kwamba – ukiendelea kutupigia kelele zako hizo – uhai wako utaupoteza mara moja. Alizingatia onyo hilo, na kunyamaza kimya.

·         Labani mmiliki wa miungu – kwa ghadhabu na chuki alimfuatilia Yakobo – Mwz 31 : 22 – 35 ni kwa sababu Mungu alipunguza spidi yake kwa kumwambia Labani kwamba, ajihadhari asimwambie Yakobo neno la shari au la amani. Lakini hata hivyo hakuacha kumfuatilia Yakobo. Unaona wazi kuwa, Mungu wa Yakobo asingeingilia kati, bila shaka Yakobo angeshindwa. Lazima uwe na uhakika na Mungu wako kwa kila hatua unayoichukua.

·         Wamiliki wa miungu wa mji wa Yoashi – kwa mioyo yenye madhara walimfuatiatilia kwa umakini mtumishi wa Mungu Gidioni – Waamuzi 6:25 – 30 walifanya uchunguzi na kupeleleza, wakagundua kwamba anayepaswa kufuatiliwa ni Gidioni.

·         Wamiliki wa mawakala wa Artemi Mungu mke wa Efeso walimfuatilia na kumuanzishia ghasia Mtumishi wa Mungu Paulo – Matendo 19 : 23 – 28, kwa sababu ya nguvu waliyokuwa nayo mji wote ulitikisika hali ya hewa ya mji ikabadilika.





1.      Yezebeli
2.      Mika asiyeokoka
3.      Labani
4.      Wenyeji wa mji wa Yoashi
5.      Wamiliki na mawakala wa Artemi mungu mke wa Efeso.
                       Hawa ni moja ya mifano hai ya kukufanya wewe kuelewa kuwa, wapo wamiliki wa
            miungu wanaofuatilia kanisa.

·         Siri ya kuwashinda ni rahisi na nyepesi.
1.    Usiwe muoga – kwa kuwa una uhakika kwamba aliye ndani yako ni mkuu kuliko miungu iliyo ndani yao.
-          Eliya hakulikumbuka jambo hilo. Alikimbia.

2.    Usiwe na kitu chochote cha miungu kwenyemaisha yako (au vitu vilivyowekwa wakfu kwa miungu)
-          Hii inamaanisha, hata tabia mbaya – imewekwa wakfu kwa miungu, mfano – ukorofi, wivu, hata kutokujali haki za wengine. Hivyo vyote ni wakfu kwa miungu ukiwanavyo – lazima wamiliki wa miungu watakuandama na kukupigia makelele yakiwemo magonjwa na wachawi.

3.    Kwa kuwa wanaweza kuyamaliza kabisa maisha yako kwa kukosa kwako umakini na usikivu.
-          Basi inabidi uwe wakfu kabisa kwa Mungu mkuu ambaye jina lake ni BWANA WA MAJESHI na MTAKATIFU WA ISRAELI.

-          Uwe wakfu – maana yake ujitoe hasa kwa kudhamiria na kuwa tayari kukabiliana na hatari yoyote ilimradi unatimiza wajibu wa kumtumikia Mungu.

MAOMBI
1.      Kila kamanda wa kikosi na jeshi kubwa la miungu, Roho Mtakatifu atawasambaratisha mara moja wakati nikiomba – kwa Jina la Yesu Kristo.

2.      Giza kubwa toka mbinguni, funika nyuso za wamiliki wa miungu wanaonifukuza katika ulimwengu wa Roho katika Jina la Yesu Kristo.

3.      Maombi yangu, poozesha kabisa nguvu za wamiliki wa miungu wanaotumia vifaa vyao vya siri kunyonya nguvu ya maombi ndani yangu – kwa Jina la Yesu Kristo.

·         Melekezo
1.      Maisha ya kujichanganya na dhambi kwa namna Fulani – mfano, kukosa uaminifu kwa namna yoyote ile, uongo wa siku moja moja, tamaa ya uzinzi na malumbano ya kila mara yasiyo na sababu kwenye familia – hayo yanaweza kukuweka kwenye nafasi ya hatari sana – kwani unakuwa  mahali ambapo, mkuki wa wamiliki wa miungu unaweza kukupata muda wowote.

v  ONYO!!!
Umekatazwa kutoa copy ujumbe ulioko kwenye karatasi hii ili kumpa mwingine,isipokuwa umeruhusiwa kumchukulia rafiki yako karatasi yake mwenyewe. Itakuwa dhambi ya makusudi ya kutokutii usipo zingatia onyo hili.

AMINA!!!!.

Comments

Popular posts from this blog

NENO LAUFUNUO LA LEO tazama Ayubu 8:7"Tena ujapokuwa huo mwanzo wako ulikuwa mdogo,lakini mwisho wako ungeongezeka sana"NENO LA UFUNUO LASIKU YAKO LEO. MUNGU ANAKUTAKA USIWE NAMAWAZO YA KUDHARAU MWANZO WAKOMDOGO. KWAMAANA TABIA YA MUNGU NIKWAMBA,YEYE HUWA HAUDHARAUMWANZO MDOGO. HATAKAMA NIMWANZO MDOGO YEYE HATAUDHARAU. "Mungu alianza na mwanadamu mmoja,leo hii wako mabilioni. Yesu alianza na wanafunzi kumi nawawili,leohii anawafuasi wengi hata hawana idadi maanawengine walishatangulia mbinguni. Historia yamakanisa mengi Africa na ulimwengu kwaujumla,yalianza namwazo mdogo sana lakini yamekuwa makubwa nayakushangaza."KILA MWANADAMU CHINI YAJUA ANAPITIA UZOEFU HUU WA KIPINDI CHAMWANZOMDOGO.LEO INABIDI UJIULIZE UKO KWENYEMWANZOMDOGO WAJAMBO GANI? JE UKO KWENYE MWANZOMDOGO WA KUANZISHA KAZI YAMUNGU? JE UKO KWENYEMWANZOMDOGO WANDOA? UKO KWENYEMWANZO WABIASHARA? UKO KWENYE MWANZO WA OFISI MPYA? UKO KWENYE MWANZO WAUCHUMBA? UKO KWENYE MWANZO WA AJIRA? UKO KWENYE MWANZO GANI? TAZAMA zekaria 4:10"maana ninani aliyeidharau siku yamambo madogo?.....OK. UNAONYWA! USIDHARAU MWANZO MDOGO ULIO NAO LEO. USIVUNJWE MOYO NAMWANZO MDOGO. USIKATISHWETAMAA NAMWANZO MDOGO.USIJIWAZIE VIBAYA KWASABABU YA MWANZO WAKO MDOGO. LEO,PIGA MOYO WAKO KONDE UCHANGAMKE MWISHO WAKO NIMZURI. MWISHO WAKO NIMKUBWA. POKEA NENO HILI LAUFUNUO ALILO KUTUMIA MUNGU SIKU YALEO.JITAHIDI UJE KANISANI UPATE MAELEKEZO ZAIDI. HUDUMA YA NENO LAUFUNUO CHINI YA MWANGALIZI MKUU MWL NA MTUME ARAM J.KAYENGELA IMEFANYIKA BARAKA SANA YAKIROHO NAKIMWILI KWAWOTE WALIO FANIKIWA KUJIUNGA RASMI. NIHUDUMA YAKIROHO YENYE UHUISHO MPYA KATIKA SIKU HIZI ZA HATALI AMBAZO KANISA LIMESAHAU UPENDO WAKWANZA.KANISA LIMEPOA.WATU WAKO MOTO KISIASA ILA KIROHO WAMEPOA KABISA.NINYAKATI ZA YEYE ALIYE NASIKIO AYASIKIE HAYA AMBAYO ROHO ANAYAMBIA MAKANISA.HERI MWENYE SIKIO LAKUSIKIA SASA. NIMUDA WAKO WAKUJA KWENYE NENO LAUFUNUO IKIWA ULIMUULIZA MUNGU AKUONYESHE NIWAPI UENDE. SIMAMA KWAMIGUU YAKO NAUCHUKUE HATUA. 0763359745/0712583194

MFULULIZO WA MAFUNDISHO YA APOSTLE ALAM J. KAYENGELA KWENYE KONGAMANO LA SIKU NANE ARUSHA TANZANIA (TAREHE 5-12 MWAKA 2013)

KUJUA KUTEMBEA NA MUNGU NIPAMOJA NAKUJUA KUSOMA ALAMA ZA NYAKATI KATIKA ROHO