Leoleoplus,com

MFULULIZO WA MAFUNDISHO YA APOSTLE ALAM J. KAYENGELA KWENYE KONGAMANO LA SIKU NANE ARUSHA TANZANIA (TAREHE 5-12 MWAKA 2013)


SIKU YA 2:

MIUNGU NA CHIMBUKO LAKO
·         Harakati za miungu bado hazijapunguzwa spidi bado zinasonga mbele kwa mwelekeo maalumu. Kwa kadiri usivyojua namna ya kushughulika na chimbuko lako, ni kwa kadiri hiyo hiyo inavyokuwa vigumu kuishinda miungu hasa iliyokuwepo katika mazingira ya chimbuko lako.

·         Kwa mfano – Moabu na kizazi chake.

-          Katika 2 Wafalme 23 : 13 na 1Walfalme 11 : 7 Moabu hakujua kwa nini – Kemoshi amekuwa Mungu wake. Hakujua. Alishituka Mungu wake akiwa Kemoshi. Hata ikajulikana kote kwamba, Kemoshi ni mungu  wa Wamoabu.  Mungu Kemoshi alimtenga Moabu na Mungu wa Israeli ambaye jina lake ni BWANA WA MAJESHI AU MOTO ULAO.

·         Mungu Kemoshi aliweza kumkamata na kumteka Moabu kutokana na chimbuko lake. Hasa chimbuko la kuzaliwa.
-          Ukisoma vizuri katika Mwz 19 : 30 – 38 Lutu alikuwa na mabinti wawili (mkubwa na mdogo) mkubwa akamshauri mdogo kwamba, wafuate desturi ya dunia yote ya uzinzi ili kuleta uzao – Mst 31. Wana wa Mungu aliye hai, tumezuiliwa kufuata desturi ya kidunia – Efeso 2 : 1 – 3, kwani kufanya hivyo kunakufanya uwe mwana wa laana. Bila kujua, binti wa Lutu waliipitia njia hiyo wakatengeneza chimbuko la laana. Pale walipozini na baba yao kwa makusudi. Nia yao ilikuwa nzuri lakini imelaaniwa. Miungu ilifuatilia tukio hili kwa ukaribu sana.

-          Binti mkubwa wa Lutu akabeba mimba toka kwa baba yake (mimba ya uziznzi) akazaa mtoto akamwita MOABU siku ileile Moabu alipozaliwa, bila kuchelewa miungu ilikuwa tayari imemuwekea alama. Moabu ndiye baba wa Wamoabi, kizazi chote na ukoo wote wa Moabu ulifunikwa na giza la miungu kwa sababu ya chimbuko lake.

-          Binti mdogo wa Lutu naye alipobeba mimba ya uzinzi akazaa mtoto na kumpa jina la Benami, ambaye ndiye baba wa Waamoni mpaka leo.

-          Mungu alijifanya kama vile hazioni nyakati hizo na akamzuia mtumishi wake Musa asije akayasumbua au kushindana na makabila hayo mawili Kumb. 2 : 9 na Mst.19.




-          Mungu anazungumzia nini kuhusu kizazi cha chimbuko la uzinzi? Ktk Hosea 2 : 4 anasema – sitawaonea rehema watoto wake, kwa maana ni watoto wa uzinzi – Mtoto wa uzinzi au mtoto aliyezaliwa kwa uzinzi, hapati rehema asipoomba rehema. Aombe rehema juu ya chimbuko lake.

·         Mahusiano ya kitovu na chimbuko lako, Ezekieli 16 : 1 – 6.
1.      Siku ile uliyozaliwa kitovu chako hakikukatwa – maana yake bado kimeunganishwa na chimbuko lako la asili. Inategemea wazazi wako walikuwa na miungu gani wakati ulipozaliwa – lakini miungu ya chimbuko lako inakukumbuka.

·         FANYA MAOMBI HAYA:
1.      Ee Mungu Mtakatifu wa vizazi vyote unayejua chimbuko langu tokea mbali, siku za kuzaliwa kwangu ulipita ukaniona nikigaagaa katika damu yangu mwenyewe, sauti yangu ikuwasilie masikioni mwako kwa sababu ya Damu takatifu ya Yesu Kristo iliyohai unirehemu kutokana na chimbuko langu – katika Jina la Yesu.

2.      Damu ya Yesu Kristo – Safisha kabisa kitovu changu leo – katika Jina la Yesu Kristo.

3.      Damu ya Yesu Kristo – Usiruhusu uovu wa baba yangu na mama yangu kuniandama leo, kwa kuwa  mtoto hatachukua uovu wa mzazi wake wala mzazi hata chukua uovu wa mtoto wake– katika Jina Yesu Kristo.

MAELEKEZO:
1.      Mwambie Roho Mtakatifu akukwamue kule ulikokwama kwenye chimbuko lako.

2.      Jifunze kuwa unafanya maombi mara kwa mara – maombi yanayoshughulikia chimbuko lako na kitovu chako.



v  ONYO!!!
Umekatazwa kutoa copy ujumbe ulioko kwenye karatasi hii ili kumpa mwingine,isipokuwa umeruhusiwa kumchukulia rafiki yako karatasi yake mwenyewe. Itakuwa dhambi ya makusudi ya kutokutii usipo zingatia onyo hili.


AMINA!!!!.


Comments

Popular posts from this blog

NENO LAUFUNUO LA LEO tazama Ayubu 8:7"Tena ujapokuwa huo mwanzo wako ulikuwa mdogo,lakini mwisho wako ungeongezeka sana"NENO LA UFUNUO LASIKU YAKO LEO. MUNGU ANAKUTAKA USIWE NAMAWAZO YA KUDHARAU MWANZO WAKOMDOGO. KWAMAANA TABIA YA MUNGU NIKWAMBA,YEYE HUWA HAUDHARAUMWANZO MDOGO. HATAKAMA NIMWANZO MDOGO YEYE HATAUDHARAU. "Mungu alianza na mwanadamu mmoja,leo hii wako mabilioni. Yesu alianza na wanafunzi kumi nawawili,leohii anawafuasi wengi hata hawana idadi maanawengine walishatangulia mbinguni. Historia yamakanisa mengi Africa na ulimwengu kwaujumla,yalianza namwazo mdogo sana lakini yamekuwa makubwa nayakushangaza."KILA MWANADAMU CHINI YAJUA ANAPITIA UZOEFU HUU WA KIPINDI CHAMWANZOMDOGO.LEO INABIDI UJIULIZE UKO KWENYEMWANZOMDOGO WAJAMBO GANI? JE UKO KWENYE MWANZOMDOGO WA KUANZISHA KAZI YAMUNGU? JE UKO KWENYEMWANZOMDOGO WANDOA? UKO KWENYEMWANZO WABIASHARA? UKO KWENYE MWANZO WA OFISI MPYA? UKO KWENYE MWANZO WAUCHUMBA? UKO KWENYE MWANZO WA AJIRA? UKO KWENYE MWANZO GANI? TAZAMA zekaria 4:10"maana ninani aliyeidharau siku yamambo madogo?.....OK. UNAONYWA! USIDHARAU MWANZO MDOGO ULIO NAO LEO. USIVUNJWE MOYO NAMWANZO MDOGO. USIKATISHWETAMAA NAMWANZO MDOGO.USIJIWAZIE VIBAYA KWASABABU YA MWANZO WAKO MDOGO. LEO,PIGA MOYO WAKO KONDE UCHANGAMKE MWISHO WAKO NIMZURI. MWISHO WAKO NIMKUBWA. POKEA NENO HILI LAUFUNUO ALILO KUTUMIA MUNGU SIKU YALEO.JITAHIDI UJE KANISANI UPATE MAELEKEZO ZAIDI. HUDUMA YA NENO LAUFUNUO CHINI YA MWANGALIZI MKUU MWL NA MTUME ARAM J.KAYENGELA IMEFANYIKA BARAKA SANA YAKIROHO NAKIMWILI KWAWOTE WALIO FANIKIWA KUJIUNGA RASMI. NIHUDUMA YAKIROHO YENYE UHUISHO MPYA KATIKA SIKU HIZI ZA HATALI AMBAZO KANISA LIMESAHAU UPENDO WAKWANZA.KANISA LIMEPOA.WATU WAKO MOTO KISIASA ILA KIROHO WAMEPOA KABISA.NINYAKATI ZA YEYE ALIYE NASIKIO AYASIKIE HAYA AMBAYO ROHO ANAYAMBIA MAKANISA.HERI MWENYE SIKIO LAKUSIKIA SASA. NIMUDA WAKO WAKUJA KWENYE NENO LAUFUNUO IKIWA ULIMUULIZA MUNGU AKUONYESHE NIWAPI UENDE. SIMAMA KWAMIGUU YAKO NAUCHUKUE HATUA. 0763359745/0712583194

MFULULIZO WA MAFUNDISHO YA APOSTLE ALAM J. KAYENGELA KWENYE KONGAMANO LA SIKU NANE ARUSHA TANZANIA (TAREHE 5-12 MWAKA 2013)

KUJUA KUTEMBEA NA MUNGU NIPAMOJA NAKUJUA KUSOMA ALAMA ZA NYAKATI KATIKA ROHO