Leoleoplus,com

MFULULIZO WA MAFUNDISHO YA APOSTLE ALAM J. KAYENGELA KWENYE KONGAMANO LA SIKU NANE ARUSHA TANZANIA (TAREHE 5-12 MWAKA 2013)


· 
SIKU YA 1:
·         KUIFUNUA MIUNGU KWA UFAHAMU KATIKA AFRIKA NA ULIMWENGU WOTE.
Miungu ni nini?
Ø   Kwa ufupi na rahisi : miungu ni roho isiyoonekana ambayo mara nyingi hukaa kwenye vitu vinavyoonekana – Mfano Vinyago au Sanamu.

Labani  -            alimwambia Yakobo  “mbona basi umeiiba Miungu yangu?” – Mwz 31 : 22 – 30 – akimaanisha vinyago – Mst 19.

Ø  Miungu ni roho zinazoishi katika usiri na nguvu, zinatenda kazi kwa ushirika wa Majeshi mengi ya kipepo. Hazina haraka wala makosa katika kumdhibiti mtu.

Ø  Miungu inaweza kumhadaa mtu – kwamba anaweza kuimiliki wakati yeye ndiye mmlikiwa Mfano: Mwz 31 : 25 – 30 Labani, siku zote alifikiri kwamba, ile miungu ilikuwa yak wake. Lakini kumbe yeye ndiye aliyekuwa mali ya ile miungu. Hakuwa mmiliki wa miungu bali alikuwa mmilikiwa wa miungu.

Ø  Mika asiyeokoka alimiliki miungu hata akaitafutia kuhani wa kuitumikia – Waamuzi 18 : 20 – 31 katika mwili, Mika alimiliki miungu, katika roho miungu ilimmiliki Mika. miungu ilimuhadaa Mika. Tazama Mwz 35 : 2 na Mst 4 Yakobo aliwaambia watu wake

“Ondoeni Miungu migeni iliyoko kwenu………” Nao wakampa Yakobo miungu migeni yote iliyokuwa mikononi mwao, na pete zilizokuwa masikioni mwao………”
                                    
Ø  Miungu ni roho zinazoweza kujificha kwenye, pete za masikioni (Heleni) kwenye kitu cha mkononi – Mfano Saa, Bangili, Pete N.K. – ili mradi tu vitu hivyo vimewekwa wakfu kwa miungu migeni.

1.      Heleni zilizo na miungu – kazi yake ni kuziba sikio la ndani muhusika asishawishike kumsikiliza Mungu wala kumtii.

2.      Bangili, Pete au Saa zilizo na miungu ndani yake – zitafunga mikono ya muhusika asiweze kupata mema ya Nchi kutoka kwa Mungu wa kweli.
                                                                             
3.      Mavazi machafu waliyoambiwa watu wa Yakobo – yalikuwa yale yaliyonajisiwa na Miungu – Mwz 35 : 2. Mavazi ya namna hiyo, Hukuondolea utukufu wa kweli wa ki Mungu.






·         Viwanda vingi vya nguo, Bangili, Pete,na Saa, katika Bara la Africa, ni wakfu kwa miungu. Imekuwa vigumu kanisa kuleta athari kwa shetani kwa sababu ya kumiliki vitu vilivyo na nguvu ya miungu bila kuviweka wakfu kwa Mungu wa kweli.

·         Kujua miungu ni nini, itakuwa msingi na hatua yako ya kwanza ya kutumia NGUVU YA MUNGU DHIDI YA MIUNGU.

·         ELEKEZA MOYO WAKO KWENYE MAOMBI:
1.    Mshukuru Roho Mtakatifu kwa kukufunulia ufunuo huu wa kuhusu jinsi ya kuifahamu miungu inayotesa Africa na Ulimwengu kwa ujumla.

2.    Mshukuru Roho Mtakatifu kwa sababu anavyoifanya miungu ichanganyikiwe kwa ajili yako.

3.    Mshukuru Roho Mtakatifu kwa jinsi anavyoiharibu miungu iliyokuwa imejificha kwenye vitu vyako, kama – Nguo, Saa, Bangili, Pete N.K.

4.    Tangaza kwamba : Vazi lolote nililo nalo ambalo limenajisiwa na miungu linalovuta matatizo kwenye maisha yangu halitaniletea athari TENA,  ninalilowesha kwenye bwawa la Damu ya Mwana Kondoo Yesu Kristo.


v  Maelekezo:
1.    Kusanya vitu vyote ulivyo navyo, uviweke wakfu na kuvitakasa kwa Damu ya Yesu.

2.    Kila unaponunua kitu chochote, kabla ya kukitumia – kiweke wakfu kwanza kwa Damu ya Yesu.

3.    Tafuta nafasi nzuri – vipengele hivyo 4 vya maombi uvifanye kwa kufunga na kuomba.

v  ONYO!!!
Umekatazwa kutoa copy ujumbe ulioko kwenye karatasi hii ili kumpa mwingine,isipokuwa umeruhusiwa kumchukulia rafiki yako karatasi yake mwenyewe. Itakuwa dhambi ya makusudi ya kutokutii usipo zingatia onyo hili.


AMINA!!!!.


Comments

Popular posts from this blog

NENO LAUFUNUO LA LEO tazama Ayubu 8:7"Tena ujapokuwa huo mwanzo wako ulikuwa mdogo,lakini mwisho wako ungeongezeka sana"NENO LA UFUNUO LASIKU YAKO LEO. MUNGU ANAKUTAKA USIWE NAMAWAZO YA KUDHARAU MWANZO WAKOMDOGO. KWAMAANA TABIA YA MUNGU NIKWAMBA,YEYE HUWA HAUDHARAUMWANZO MDOGO. HATAKAMA NIMWANZO MDOGO YEYE HATAUDHARAU. "Mungu alianza na mwanadamu mmoja,leo hii wako mabilioni. Yesu alianza na wanafunzi kumi nawawili,leohii anawafuasi wengi hata hawana idadi maanawengine walishatangulia mbinguni. Historia yamakanisa mengi Africa na ulimwengu kwaujumla,yalianza namwazo mdogo sana lakini yamekuwa makubwa nayakushangaza."KILA MWANADAMU CHINI YAJUA ANAPITIA UZOEFU HUU WA KIPINDI CHAMWANZOMDOGO.LEO INABIDI UJIULIZE UKO KWENYEMWANZOMDOGO WAJAMBO GANI? JE UKO KWENYE MWANZOMDOGO WA KUANZISHA KAZI YAMUNGU? JE UKO KWENYEMWANZOMDOGO WANDOA? UKO KWENYEMWANZO WABIASHARA? UKO KWENYE MWANZO WA OFISI MPYA? UKO KWENYE MWANZO WAUCHUMBA? UKO KWENYE MWANZO WA AJIRA? UKO KWENYE MWANZO GANI? TAZAMA zekaria 4:10"maana ninani aliyeidharau siku yamambo madogo?.....OK. UNAONYWA! USIDHARAU MWANZO MDOGO ULIO NAO LEO. USIVUNJWE MOYO NAMWANZO MDOGO. USIKATISHWETAMAA NAMWANZO MDOGO.USIJIWAZIE VIBAYA KWASABABU YA MWANZO WAKO MDOGO. LEO,PIGA MOYO WAKO KONDE UCHANGAMKE MWISHO WAKO NIMZURI. MWISHO WAKO NIMKUBWA. POKEA NENO HILI LAUFUNUO ALILO KUTUMIA MUNGU SIKU YALEO.JITAHIDI UJE KANISANI UPATE MAELEKEZO ZAIDI. HUDUMA YA NENO LAUFUNUO CHINI YA MWANGALIZI MKUU MWL NA MTUME ARAM J.KAYENGELA IMEFANYIKA BARAKA SANA YAKIROHO NAKIMWILI KWAWOTE WALIO FANIKIWA KUJIUNGA RASMI. NIHUDUMA YAKIROHO YENYE UHUISHO MPYA KATIKA SIKU HIZI ZA HATALI AMBAZO KANISA LIMESAHAU UPENDO WAKWANZA.KANISA LIMEPOA.WATU WAKO MOTO KISIASA ILA KIROHO WAMEPOA KABISA.NINYAKATI ZA YEYE ALIYE NASIKIO AYASIKIE HAYA AMBAYO ROHO ANAYAMBIA MAKANISA.HERI MWENYE SIKIO LAKUSIKIA SASA. NIMUDA WAKO WAKUJA KWENYE NENO LAUFUNUO IKIWA ULIMUULIZA MUNGU AKUONYESHE NIWAPI UENDE. SIMAMA KWAMIGUU YAKO NAUCHUKUE HATUA. 0763359745/0712583194

MFULULIZO WA MAFUNDISHO YA APOSTLE ALAM J. KAYENGELA KWENYE KONGAMANO LA SIKU NANE ARUSHA TANZANIA (TAREHE 5-12 MWAKA 2013)

KUJUA KUTEMBEA NA MUNGU NIPAMOJA NAKUJUA KUSOMA ALAMA ZA NYAKATI KATIKA ROHO