NENO LA UFUNUO LA WIKI HII KWA KANISA ULIMWENGUN-Mfano wa mtu mjinga na mpumbavu atafutaye nyoka na kujilisha mawe
UTANGULIZI
Kiongozi mkuu mwanzirishi wa Huduma ya Neno la Ufunuo iliyoko Chanika Dar es salaam Tanzania Mwalimu na Mtume Alam J.Kayengela-jana alianza kwa kusema
Nivema tuelewe kwamba mara nyingi sana Bwana YESU alifundisha kwa mifano,kila mfano ulikuwa na uhai wa uhalisia.
Ukisoma katika marko 4;2-9 unaona kwamba mkutano mkubwa wa wawatu wengi walimuendea akaanza kusema nao kwa mfano wa mpanzi aliye panda mbegu,zingine zilidondokea njia panda zingine kwenye mwamba,zingine kwenye miiba nazingine kwenye udongo mzuri-baada ya kuuelezea hivyo ule mkutano wawatu weni kasha waliondoka zao bila kupata ufunuo wa maana ya ulemfano.kabla hawajasambaa kwenda makwao mst wa 9.akawaambia Aliye na sikio la kusikilia na asikie.wakaendazao majumbani wakifurahia ule mfano wa mpanzi bila Neno la ufunuo la maana ya mpanzi yule
Ukisoma mst wa 10-20 unaliona kundi la watu wachache sana wakaenda kumuuliza maana ya mfano ule wa mpanzi.Hili nilile kundi la watu wachache sana duniani watafutao Neno la Ufunuo.Wkasema,maana yake nini mfano ule wa mpanzi? Ndipo akaanza kuwaambia kwamba,Ninyi mmejariwa kuzijua siri za ufalme wa Mungu. Akimaanisha kuwa lile kundi la watu wengi lili enda bila kuelewa chchote cha kiufunuo. Ndipo akaanza kuwafafanulia kiufunuo maana ya ule mfano wa mpanzi.
Kundi kubwa la watu duniani kiukweli wamelidhika tu,nayale mahubiri wayapatayo nahujiendea nyumbani nakusema,Leo nilikuwa kanisani na nimesikia mahubiri mazuri sana.Lakini kwakweli lile Neno lenyewe la ufunuo bado hawajalipata.Kwasababu,kulipata Neno la ufunuo kunahitaji hatua nyingine ya maamuzi.Ndiyo maana hata wewe msomaji wangu yapasa ujiulize,ikiwa huwa una pata Neno la Ufunuo au mahubiri tu.
Mtume Kayengela alisoma mathayo 7;9-10 akasema,Au kuna mtu yupi kenu ambaye mwanawe akimwomba mkate atampa jiwe? au akiomba samaki atampa nyoka?-Akasema,nimjinga tu,na mpumbavu anaye weza kufanya hivyo. Mjinga nampumbavu atafutaye nyoka na kujilisha mawe.
Kiongozi huyo alisema kwamba,mjinga na mpumbavu huamka asubuhi na kwenda kutafuta nyoka na mwenyewe hujilisha mawe.Wengine anao pishana nao bara barani wanakuwa wakitafuta asali nakujilisha asali njema na tam.Jamii yawatu majirani,marafiki,ndugu,nawapendwa wanapo kutana naye kisimani maana kunasiku huenda kisimani kisima chenye maji safi. Wanapo muona yule mjinga nampumbavu atafutaye nyoka nakujilisha mawe naye hujichangamsha mbele zao lakini yeye akiwa ameficha nyoka namawe mazito.
Wakati wa kula,kilamtu huchukua kile alicho kusanya mchana kutwa,walio kusanya asali huanza kula asali zao tam,nayule mjinga nampumbavu huanza kula vinyoka alivyo vikusanya mchana kutwa kisha kujitwika mawe yake mazito.
Baaba yakutoa mfano huo wa mtu mjinga na mpumbavu atafutaye nyoka na kujilisha mawe,Apostle Kayengela alisema,hebu kanisa fikirini kama nikisema huu ndio mwisho wa ujumbe wa leo wa mfano huu bila kutoa maana ya mfano huu utaenda na nini leo?akasema, sasa huu ndio msiba wawapendwa wengi huko nje,wamenyimwa kujua maana ya mambo furani kwasababu hawataki kulifuata nakutulia kwenye Neno la Ufunuo
MAANA YAMFANO WA MJINGA NA MPUMBAVU ATAFUTAYE NYOKA NA KUJILSHA MAWE
Mjinga nampumbavu atafutaye nyoka na kujilisha mawe niyule mbarikiwa au mpendwa ambaye hutafuta nakuwaza mambo yasiyo sahihi.Mmbo yanayo athiri moyowake
Mathayo 7;9-10 -nyoka huwakilisha mawazo mabaya na kwa upande wa mawe ndipo ukisoma mithali 27;3 mawe ni ule mzigo mzito utokanao nayalemawazo mabaya,yakujiwazia machungu,maumivu,upweke-n.k
Wale wengine walio jitafutia asali tam-niwale wabarikiwa wanao linda nafsi zao zisije zikanajisiwa namawazo ya makwazo,matusi waliyo tukanwa n.k
Jamii ya watu ,ndugu,majirani,rafiki niwale wabarikiwa wenzako au washirika wenzako. Kukutana kisimani kisima cha maji safi,kisimani ni kanisani kwako.
Wanapo muona naye hujichangamsha mbele yao,lakini yeye akiwa ameficha moyoni mwake mawazo mabaya yenye msongo mzito wa matatizo anayo pitia kila siku.
Wakati wakula kila mtu huchukua nakula kile alicho kikusanya mchana kutwa ambacho niyale mawazo uliyo yakusanya mchana kutwa,sasa wengine wanalisha mioyo yao mawazo matam kama asali lakini wewwe unailisha nafsi yako majaribu yanayo kuhangaisha nakuku taabisha moyoni,kiasikwamba unakuwa namsongo wenye shinikizo aidha la kufeli dalasani au kuvunjikiwa ndoa au umefukuzwa kazi,au maneno mabaya unayo semwa huko nje,au moyo wako unaulisha mawazo ya kuvunjika na kukata tamaasan kwasababu mshahara wako haukutoshi-Apostle Kayengela alionya kwamba,Je,hujui kwamba mafikra yako ni chakula cha nafsi yako? Kwanini nafsi yako unailisha mambo mabaya badala ya yale yakutiayo moyo na kuku fariji? kwanini unaruhusu mgandamizo wa fikwa zenye msongo wa mawazo yamambo ambayo unajua kabisa kwauwezo wako huyawezi?
Mith 17;10 kwanini unajipiga mwenyewe mapigo mia? yaani unatunia mawazo yako mabaya yakuleteayo shinikizo kujishambulia nayo.Kweli,waweza kuwa yule mjinga na mpumbavu atafutaye nyoka na kujilisha mawe.
Zaburi 4;4 anasema-Tafakarini vitandani mwenu na kutulia. Unapo tulia nakutafakari,maanayake muda huo unakuwa unailisha nafsi yako. Sasa kwanini unailisha nafsi yako makwazo badala ya matumaini?
OMBI
-SEMA KWA IMANI-Ee Jehova Mungu ambaye uko kila mahali kwa wakati wote-ninatambua uwepo wako mahali hapa,nisaidie kwa uwezowako usio wa kawaida kwani sitaki kuwa mjinga nampumbavu atafutaye nyoka nakujilisha mawe. Niunganishe na Mtandao wako wa Neno la Ufunuo. Kwahiyo nina kataa kuwa na mzigo wa mgandamizo wa shinikizo la msongo wa mawazo yashambuliao nafsi yangu KWAJINA LA YESU KRISTO WA NAZALET. AMINA. AMINA. AMINA
KWAKUFUNGULIWA ZAIDI HASA VIFUNGO VYA NAFSI-PIGA
0763359745 AU 0712583194
KARIBU SANA-TUKO CHANIKA DSM
KAYENGELA AMEKUWA AKITUMIWA SANA NA MUNGU KUWA FUNGUA SANA WA TU WENGI WA MUNGU
Comments
Post a Comment